TRA

TRA

Saturday, April 30, 2016

Farid Mussa

No comments:

Kutoka Club Deportive Tenerife Hispania kwenye majaribio ya Farid Musa wa Azam FC
Winga mshambuliaji wa timu ya taifa ya Tanzania na Azam FC Farid Musa yupo Hispania anaendelea na majaribio yake ya kutafuta nafasi ya kucheza soka la kulipwa, Farid ameendelea na majaribio yake Club Deportive Tenerife ya Hispania.
IMG-20160429-WA0016
Farid amethibitisha kuendelea vizuri kiafya lakini ameiambia millardayo.com kuwa ana siku ya nne Club Deportive Tenerife ambapo hapo anakaa wiki moja halafu anaendelea na majaribio katika vilabu vingine vya hapo Hispania alivyotafutiwa na wakala wake John Sorzano.
IMG-20160429-WA0017
IMG-20160429-WA0018

Magazeti leo

No comments:


20160430_102444
20160430_102501
20160430_102518
20160430_102539
20160430_102556
20160430_102613
20160430_102624
20160430_102632
20160430_102703
20160430_102717
20160430_102729
20160430_102750
20160430_102805
20160430_102813
20160430_102827
20160430_102839
20160430_102849
20160430_102901
20160430_102919
20160430_102926
20160430_102935
20160430_102948
20160430_103003
20160430_103012
20160430_103026
20160430_103037
20160430_103120
20160430_103146
20160430_103159
20160430_103207
20160430_103230
20160430_103238
20160430_103301
20160430_103316

BASATA KUADHIMISHA SIKU YA MUZIKI WA JAZZ

No comments:

New Picture
National Arts Council BASATA
Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa linalojishughulisha na Elimu na Sayansi (UNESCO) litaungana na wasanii mbalimbali nchini na wadau wa Sanaa kuazimisha siku ya muziki wa Jazz duniani ambayo kwa mara ya kwanza itaazimishwa nchini Mei 2, 2016.
Maazimisho hayo ambayo yatapambwa na burudani mbalimbali kutoka kwa Wasanii wa muziki wa jazz hususan Band maarufu ya Das Jazz yanatarajiwa kufanyika kwenye Ukumbi wa Baraza hilo ulioko Ofisi za BASATA Ilala Sharif Shamba jijini Dar es Salaam.
Sambamba na burudani hizo, kutakuwa na mada mbalimbali zitakazowasilishwa na wadau wa muziki huu wa jazz ambazo zitalenga kuamsha ari, thamani na ufahamu wa muziki huu maarufu duniani miongoni mwa wasanii nchini.
Wawasilishaji wa mada hizo pamoja na mada zao kwenye mabano ni pamoja na John Kitime (Matumizi ya neno Jazz), Carola Kinasha (Uhusiano kati ya Elimu ya Muziki na Jazz) na Kurwigira Mareges (Historia ya Muziki wa Jazz) na Masoud Masoud (Ujue Muziki wa Jazz)
Mbali na burudani na mada hizo kuhusu muziki huo wa Jazz kutakuwa na wageni waalikwa kutoka kwenye balozi na vituo vya Utamaduni vya nchi mbalimbali zilizopo hapa Tanzania
BASATA linatoa wito kwa wasanii na wadau wa muziki huu wa jazz kujitokeza kwa wingi katika maadhimisho haya ambayo yatakuwa yakifanyika kila mwaka sambamba na mataifa mengine duniani.
Sanaa ni kazi, tuipende na kuithamini
Godfrey Mngereza
Katibu Mtendaji – BASATA (P.T)

CHRAGG yawapiga msasa Waandishi wa habari kuhusu Mpango wa Kimataifa wa Kujitathmini juu ya Masuala ya haki za binadamu.

No comments:


Kamishna wa Tume ya Haki za Binadamu Umoja wa Mataifa, Chitralekha Massey akiwapiga msasa baadhi ya waandishi wa habari kuhusu Mpango wa Kimataifa wa Kujitathmini juu ya Masuala ya Haki za Binadamu (UPR) wakati wa warsha ya siku moja 29 Aprili 2016 Mkoani Morogoro.
Kamishna wa Haki za Binadamu na Utawala Bora, Bi. Salma Ally Hassan (kulia) akifafanua jambo kwa waandishi wa habari kuhusu Mpango wa Kimataifa wa Kujitathmini juu ya Masuala ya Haki za Binadamu (UPR) wakati wa warsha ya siku moja 29 Aprili 2016 Mkoani Morogoro.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dkt. James Jesse akitoa mada mbele ya waandishi wa habari kuhusu Mpango wa Kimataifa wa Kujitathmini juu ya Masuala ya Haki za Binadamu (UPR) wakati wa warsha ya siku moja 29 Aprili 2016 Mkoani Morogoro.



Afisa Utetezi na Haki za Binadamu wa Shirika la Under The Same Sun (UTSS) Bi. Perpetua Senkoro akitoa mada kuhusu masuala ya watu wenye ulemavu kupewa haki zao wakati warsha ya siku moja kuhusu Mpango wa Kimataifa wa Kujitathmini juu ya Masuala ya Haki za Binadamu (UPR) wakati wa warsha ya siku moja 29 Aprili 2016 Mkoani Morogoro.




Wadau wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora wakiwa katika picha ya pamoja na Waaandishi wa Habari waliohudhuria mafunzo ya siku moja ya warsha kuhusu Mpango wa Kimataifa wa Kujitathmini juu ya Masuala ya Haki za Binadamu (UPR) wakati wa warsha ya siku moja 29 Aprili 2016 Mkoani Morogoro.

(Picha zote na Benedict Liwenga)



Na Benedict Liwenga.


Asasi za Kiraia pamoja na Taasisi za kutetea haki za binadamu nchini zimewaasa Waandishi wa Habari nchini kujikita katika kuhabarisha umma kuhusiana na masuala ya haki za binadamu ikiwemo mauaji ya watu wenye ualbino, mauaji ya vikongwe, ukatili dhidi ya watoto, pamoja na adhabu ya vifo.

Rai hiyo imetolewa leo na Kamishna wa Haki za Binadamu na Utawala Bora, Bi. Salma Ally Hassan wakati wa Warsha ya siku moja iliyofanyika mkoani Morogoro yenye lengo la kuwajengea uelewa Wanahabri kuhusu Mpango wa Kimataifa wa kujitathmini juu ya Masuala ya Haki za Binadamu (UPR).

Bi. Salma ameeleza kuwa kutokana na tathmini ya masuala ya haki za binadamu nchini, vyombo vya habari havinabudi kuwa na uelewa mkubwa kuhusu umuhimu wa kuziongelea haki za binadamu kwani jamii imekuwa haizitambui baadhi ya haki hizo na kumekuwepo na kukithiri kwa vitendo vya uvunjifu wa amani yakiwemo matukio ya mauaji ya watu wenye ualbino, vikongwe pamoja na ukatili kwa watoto.

Ameongeza kuwa, baadhi ya watu nchini wamekuwa wakijichukulia sheria mkononi kwa kuua watu ambapo watu wenye kuyasemea hayo ni Vyombo vya Habari lengo likiwa ni kukemea kuendelea kwa vitendo hivyo.

“Uvunjaji wa haki za binadamu unafanywa na watu katika jamii, kwa mfano, mauaji ya Watu wenye Ualbino, mauaji ya vikongwe, pale sio Serikali inakua imevunja haki za binadamu, bali ni watu katika jamii”, alisema Bi. Salma.

Kwa upande wake Mshauri wa masuala ya haki za binadamu kutoka Ofisi ya Umoja wa Mataifa nchini Tanzania, Bi. Chitralekha Massey ameeleza kuwa, ni vema Tanzania ikakubalina na mapendekezo yanayohusiana na masuala ya haki za binadamu yanayoendana na Dunia kwa ajili ya ulinzi wa haki hizo.

“Sisi kama Umoja wa Mataifa tunapenda kuona Tanzania inafanya uamuzi utakaosaidia kuboreshwa kwa haki za binadamu nchini kwani ni wakati sasa wa jamii kusema kwa uwazi kuwa mapendekezo hayo yatakuwa yenye manufaa kwao”, alisema Massey.

Aidha, katika warsha hiyo, vyombo vya habari, jamii pamoja na Serikali wanajukumu la kulinda haki za binadamu na kuendelea kukemea matukio yanayovunja amani katika jamii.

Tarehe 9 Mei, 2016 Tanzania inatarajiwa kufanyiwa tathmini ya pili juu ya hali ya haki za binadamu nchini na Nchi Wanachama wa Umoja wa Mataifa ambapo tayari Asasi za Kiraia na Watetezi wa haki za binadamu wamekwisha wasilisha mapendekezo yao kwa Wawakilishi wa nchi wanachama wa umoja huo.

SHAKA ITAKA MIKOA YA KASKAZINI KUKATAA SIASA ZA UKANDA NA UZAWA

No comments:



Kaimu Katibu Mkuu uvccm Taifa SHAKA HAMDU SHAKA akikabidhi kadi kwa wanachama wapya wilaya ya Mwanga

Kaimu katibu mkuu UVCCM taifa Shaka Hamdu Shaka akifungua shina la wakereketwa wa CCM katika kijiji cha Mtalang'a
kikundi cha ngoma kutoka katika kabila la kichaga kikitumbuiza wakati wa kaimu katibu mkuu wa UVCCM akiwasili wilayani Mwanga 
 
Na Woinde Shizza, Mwanga

Umoja wa vijana wa Chama cha mapinduzi umewataka wananchi wa mikoa ya Kaskazini mwa Tanzania kukataa na kuzikwepa siasa za uzawa na ukanda kwasababu ubaguzi ni dhambi isiyosamehewa na mungu.

Wametakiwa kutambua kuwa ubaguzi ni zaidi ya laana ambayo ikiemea na kujengeka katika jamii kuiondosha kwake ni kazi ngumu na kwamba kafara yake lazima maisha ya watu yapotee au damu imwagike.

Hayo yameelezwa leo na Kaimu katibu mkuu wa UVCCM Shaka Hamdu shaka wakati akizungumza na wanachama wa CCM katika kijiji cha Mtalang'a kata ya Mwanga mkoani hapa.

Shaka alisema ni aibu binadamu aliyestaarabika, kupata elimu akawa anaishi, kupigania madaraka., vyeo au utawala kwa kutumia maneno au sera za ubaguzi wa dini, ukabila, uzawa au ukanda.

Aidha aliongeza kuwa baada ya miaka 52 ya uhuru na Muungamo wa mataifa ya Tanganyika na zanzibar, anapotokea kiongozi au chama cha siasa kinachofanya shughuli za kisiasa kwa kueneza sumu ya uzawa na watu kupiga kura kwa ukanda ni hatari mpya mbele ya watanzania.

"Ndugu zangu wananchi wa mikoa ya Kaskazini kuna hatari inawanyemelea, msipoitahadhari na kukwepa, ikiwaingia kutoka kwake ni mbinde, ili ifanyike kafara ya kuondoa laana hiyo si ajabu damu ikanwagika "alisema Shaka

Alisema wakati baadhi ya wananchi wa mikoa hiyo wakiaza kughilibiwa na wanasiasa uchwara wakubali kuchagua vyana kwa sababu za ukanda na ukabila, idadi kubwa ya wakaazi wa Mikao hiyo wanaishi na wamejijenga kiuchumi katika mikoa mingine ya nchi na huko hawabughudhiwi wala kubaguliwa.

"Haiikisha mkiendela kubagua wenzetu na nyinyi mtaanza kubaguliwa,vdhambi ya ubaguzi haina toba, kataeni siasa chafu na wakwepeni matapeli wa kisiasa na walafi wa madaraka "alisisitiza shaka.

Kaimu huyo katibu mkuu wa UVCCM alisema kwamba Taifa la Tanania halikuachwa na wakoloni bali liliundwa na waasisi wake Marehemu baba wa Taifa Mwalimu julius Nyerere na Hayati Mzee Abeid Amani Karume bila na kupiga vita ubaguzi wa kikabila, udini, rangi za watu au kuendekeza uzawa.

Alisema kutendo chochote kitakachopelekea kuacha au kuipuuza misingi ya Taifa letu ambayo imewafanya watu kuwa na umoja, upendo na mshikamano radhi za waasisi hao pamoja na za wenzao zitaigeukia nchi yetu iwapo tutakubali kugawanywa na wanasiasa wachovu.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa uvccm mkoa wa kilimanjaro Juma Raib Juma alisisitiza haja ya kuendelea kuheshimu na kudumisha umoja wa kitaifa nchini na mwanasiasa yeyote atakayeonekaa kana ni mkabila, mdini na asiyehimiza amani na utulivu aogopwe kama ebola.

"Ni mkoa upi leo hii nchini kwetu ambao wanaishi janii ya watu wa kabila moja,dini moja,rangi moja au ukoo mmoja,tikate ukabila ns vyama vilivyoanza kuonyesha ubaguzi wa aina yeyote "alisema Raibu

Mwenyekiti huyo wa UVCCM mkoani kilimanjaro alisema vyama vinavyopita na kueneza siasa za chuki, ukanda au ukabila vichunguzwe na ikiwa vitatjibiiyika kujihusisha na vitendo hivyo hatari Msajili wa Vyama vya siasa nchini achukue hatua za kisheria kuifuta mara moja kabla havijaleta madhara.

Shaka na msafara wake wanaendelea na ziara katika wilaya ya Mwanga kabla ya kuhitimisha wilaya ya Same baadae kuelekea
Mkoani Tanga.
 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger