TRA

TRA

Sunday, July 31, 2016

Magazeti ya Leo

No comments:
IMG_20160801_045521
IMG_20160801_045536
IMG_20160801_045554
IMG_20160801_045609
IMG_20160801_045624
IMG_20160801_045640
IMG_20160801_045658
IMG_20160801_045728
IMG_20160801_045757
IMG_20160801_045814
IMG_20160801_045828
IMG_20160801_045844
IMG_20160801_045904
IMG_20160801_045917
IMG_20160801_045934
IMG_20160801_045955
IMG_20160801_050015
IMG_20160801_050040
IMG_20160801_050101
IMG_20160801_050116
IMG_20160801_050132
IMG_20160801_050148
IMG_20160801_050204
IMG_20160801_050225
IMG_20160801_050238
IMG_20160801_050258
IMG_20160801_050317

RAIS WA SIMBA, AVEVA AKITANGAZA MKUTANO KURIDHIA KUFANYA MABADILIKO

No comments:


evans aveva
Chanzo Mo Blog
Hatimaye ile ndoto ya mashabiki wa klabu ya Simba kuona klabu yao ikibadili mfumo unaotumika sasa wa wanachama ndiyo kuwa wamiliki wa klabu na kuingia katika mfumo wa kampuni imekamilika.
Hilo limethibitishwa na Rais wa Simba, Evans Aveva katika mkutano mkuu wa Simba ambao ulikuwa unafunga msimu wa 2015/2016 kwa kutolewa taarifa na kuweka mipango mipya kwa msimu ujao.
Hatua hiyo imekuja baada ya mmoja wa mashabiki wa Simba na Mkurugenzi Mtendaji na Rais wa makampuni ya Mohammed Enterprises, Mohammed Dewji “MO” kutangaza nia ya kutaka kununua hisa za asilimia 51 na kutoa Bilioni 20 kwa ajili ya kuisaidia Simba kurudi katika makali yake ikiwa ni pamoja na kusajili wachezaji wazuri, kocha mzuri, kujenga kiwanja, kuweka vituo vya kukuzia vipaji vya Simba na vingine vingi.
Kutokana na jambo hilo, mashabiki wa Simba walionekana kuvutiwa na mipango ya MO na hivyo kuandamana katika ofisi za klabu na kushinikiza uongozi kukubaliana na MO ili kununua hisa na kuanza kuwekeza ili Simba irudi katika makali ya kushinda mataji.
Ipo hapa video ikimuonyesha Rais wa Simba, Evans Aveva akitangaza mkutano wa Simba kuridhia kufanya mabadiliko.

RADIO MARIA WAIOMBA SERIKALI KUREKEBISHA SHERIA YA LESENI YA REDIO ZA JAMII

No comments:



maki1
Mwashamu Askofu wa Jimbo Katoliki la Mtwara akikata keki wakati wa sherehe za kilele cha maadhimisho ya miaka 20 ya Redio Maria Tanzania jana Jijini Dar es Salaam. Kutoka kushoto ni Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Anne Makinda, katikati ni Mkurugenzi wa Redio Maria Tanzania (RMTZ) Padre John Maendejana.
maki2
Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Anne Makinda akikata keki wakati wa sherehe za kilele cha maadhimisho ya miaka 20 ya Redio Maria Tanzania jana Jijini Dar es Salaam yaliyoanza rasmi tangu April 26 mwaka huu. Katikati ni Mwashamu Baba Askofu wa Jimbo Katoliki la Mtwara Titus Mdoe,kutoka kulia ni Mhamasishaji Mkuu wa Redio Maria Tanzania Bi. Veronica Mwita na wapili kushoto ni Mkurugenzi wa Redio Maria Tanzania (RMTZ) Padre John Maendejana.
maki3
Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Benjamin William Mkapa akisalimiana na Baba Askofu wa Jimbo Katoliki la Mtwara Mwashamu Askofu Titus Mdoe wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 20 ya Redio Maria Tanzania jana Jijini Dar es Salaam.Katikati ni Mkurugenzi wa Redio Maria Tanzania Padre. John Maendejana.
maki4
Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Saalam Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo akizungumza na wadau na marafiki wa Redio Maria Tanzania jana Jijini Dar es Salaam wakati wa hafla ya kuadhimisha miaka 20 tokea kuanzishwa kwa Redio hiyo
maki5
Mkurugenzi wa Redio Maria Tanzania Padre John Maendeleo akizungumza na wadau na marafiki wa Radio Maria Tanzania jana Jijini Dar es Salaam wakati wa hafla ya kuadhimisha miaka 20 tokea kuanzishwa kwa Redio hiyo.
maki6
Rais wa Redio Maria Tanzania Humphrey Julius Kira akizungumza na wadau na marafiki wa Radio Maria Tanzania jana Jijini Dar es Salaam wakati wa hafla ya kuadhimisha miaka 20 tokea kuanzishwa kwa Redio hiyo.
maki7
Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Anne Makinda akipokea risala kutoka kwa Rais wa Redio Maria Tanzania Humphrey Julius Kira(Kulia) wakati wa sherehe za kilele cha maadhimisho ya miaka 20 ya Redio Maria Tanzania jana Jijini Dar es Salaam.
maki8
Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Anne Makinda akipeana mkono na baadhi ya marafiki wa Redio Maria Tanzania waliofika kuchangia Redio hiyo katika harambee iliyofanyika ikiambatana na sherehe za maadhimisho ya miaka 20 ya Redio Maria Tanzania jana Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Rais wa Redio Maria Tanzania Bw. Humphrey Julius Kira.
maki9
Baadhi ya waumini wa Roman Katoliki wakifurahi wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 20 ya Redio Maria Tanzania (RMTZ). Picha zote na Frank Shija, MAELEZO.
Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO
Rais wa Redio Maria Tanzania, Humphrey Kira ameiomba Serikali kurekebisha Sheria ya leseni ya redio za jamii ili ziweze kuwa na vituo vingi vya kurushia matangazo yake.
Hayo yamesemwa jana na Rais huyo wakati alipokuwa akisoma risala kwenye sherehe za kilele cha maadhimisho ya miaka 20 ya redio hiyo yaliyofanyika kwenye viwanja vya Msimbazi Centre, Jijini Dar es Salaam.
Kira amefafanua kuwa redio za kijamii hasa zilizojikita katika nyanja za kiimani zinasaidia kufundisha maadili na kufanya wananchi wakomae kiimani, hivyo angefurahi sana kuona redio za aina hiyo zinapewa leseni za kurusha matangazo yake nchi nzima.
“Ndugu mgeni rasmi, redio yetu inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na ufinyu wa sehemu za usikivu (coverage areas) ambapo tatizo hili linatokana na sheria ya leseni za redio ambayo hairuhusu redio za aina hiyo kuwa na vituo zaidi ya kumi nchini nzima, tunaomba serikali itusaidie kuiboresha sheria hii ili tuongeze vituo vya matangazo ya dini”, alisema Kira.
Rais huyo ameongeza kuwa majimbo yote yanahitaji kufikiwa na huduma za maombi, hivyo anawashauri wasikilizaji wote kuendelea kuisikiliza redio hiyo kwa njia ya mitandao ikiwemo simu za mkononi kwani hivi sasa huduma hiyo inapatika nchi nzima.
Kwa upande wake Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo ametoa rai kwa uongozi wa redio hiyo kutobadilisha maudhui wala kuweka vipindi visivyokuwa vya dini ili iendelee kuunganisha familia na sio kuzigawa familia.
“Tunasema kuwa redio Maria ni sauti ya kikristu nyumbani mwako lakini mimi nasema ni sauti ya Mungu ndani ya familia kwa kuwa inafanya kazi ya kuunganisha familia, vyombo vingine vya habari vinafanya kazi kubwa ya kuigawa familia lakini Redio Maria ni tofauti”, alisema  Pengo.
Askofu Pengo amewashukuru wananchi wote waliohudhuria kwenye maadhimisho hayo kwa kuwa kufanya hivyo ni njia moja wapo ya kumuenzi na kumpa heshima Mama Bikira Maria.
Nchini Tanzania, Redio Maria ilianzishwa Aprili 26 mwaka 1996 katika Jimbo Kuu Katoliki la Songea ikiwa na lengo la kumsaidia Mama Bikira Maria katika kazi yake ya kumtangaza Yesu Kristo kwa watu wote. Mpaka sasa ina vituo 10 Tanzania Bara na viwili Zanzibar. (P.T)

RAIS DKT. MAGUFULI AFANYA MKUTANO TINDE, ISAKA NA KAHAMA MKOANI SHINYANGA

No comments:


M1
Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia mamia wa wakazi wa Kahama mara baada ya kuwasili akitokea Nzega mkoa Tabora.
M2
Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Pombe Magufuli akicheza jukwaani wimbo wa kwaya ya Haleluya Kuu kutoka Kanisa la KKKT-Usharika wa Yeru Ndala Shinyanga kabla ya Kuhutubia mamia ya wakazi Kahama mkoani Shinyanga.
M4
Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Mbunge wa zamani wa Kahama James Lembeli mara baada ya kuwasalimia wananchi waliofika kwa ajili ya kumsikiliza Rais katika viwanja hivyo vya Kahama.
M5
Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia mamia wa wakazi wa Isaka mkoani Shinyanga.
M7
Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Pombe Magufuli akiwa ameambatana na Mbunge wa zamani wa Kahama James Lembeli ambaye ni mwanachama wa Chadema mara baada ya kumaliza kuhutubia mkutano mjini Kahama mkoani Shinyanga.
M8
Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Pombe Magufuli akicheza pamoja na Wanakwaya wa Haleluya Kuu kutoka Kanisa la KKKT-Usharika wa Yeru Ndala Shinyanga mara baada ya kumaliza kuhutubia mkutano Kahama mjini mkoani Shinyanga.
M9
Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia mara baada ya kuoneshwa picha na kijana mmoja aliyeishika picha hiyo.
M10
Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia mamia ya wakazi wa Tinde mkoani Sinyanga.
PICHA NA IKULU (P.T)

ESRF YAWAKUTANISHA WADAU MBALIMBALI KUICHAMBUA BAJETI YA SERIKALI KATIKA SEKTA YA AFYA NA VIWANDA

No comments:


Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Jamii, (ESRF), Dkt.Tausi Kida, akitoa hotuba ya ufunguzi wa mdahalo uliolenga kujadili changamoto zinazoikabili bajeti ya mwaka 2016/2017 kwenye sekta ya Afya na Viwanda, kwenye makao makuu ya ESRF jijini Dar es Salaam. Mdahalo huo umewakutanisha wasomi, wawakilishi wa Taasisi za Umma na Binafsi. (Picha zote na K-VIS MEDIA/Khalfan Said).
TAASISI ya Utafiti ya Uchumi na Jamii (ESRF) imewakutanisha wasomi na wawakilishi wa taasisi za umma na kibinafsi kuchambua bajeti ya Serikali ya mwaka 2016/2017 katika Sekta ya Afya na Viwanda ili kuona inavyoweza kutatua changamoto zinazokabili Sekta hizo kwenye mdahalo uliokutanisha wasomi, wawakilishi wa Taasisi za Umma na Binafsi na kufanyika makao makuu ya Taasisi hiyo jijini Dar es Salaam.
Akifungua mdahalo huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo, Dkt.Tausi Kida alisema, Taasisi yake imeona ni vema kuwakutanisha wadau kujadili bajeti hiyo katika sekta ya Afya na Viwanda, kwa vile zinagusa uchumi wa wananchi.
Akiwasilisha mada juu ya bajeti ya Serikali 2016/2017na changamoto zinazoikabili sekta ya Afya, Mhadhiri wa Chuo Kikuu Kishiriki Cha Afya na Sayansi Shirikishi, Cha Muhimbili, (MUHAS), Profesa Phares Mujinja alisema, ingawa bajeti iliyotengwa kwenye sekta ya Afya ni kubwa, lakini bado kuna changamoto kadhaa kwa vile Wizara hiyo imepanuka kutokana na kuhudumia maeneo mengi.
Profesa Mujinja alitolea mfano wa ununuzi wa madawa ambapo, zaidi ya asilimia 90 ya madawa yanayotumika huagizwa kutoka nje na hivyo fedha nyingi za kigeni hutumika.
Katika majumuisho yake, Profesa Mujinja alisema, ni vema Serikali ielekeze nguvu zake kwenye uanzishwaji wa viwanda vya kuzalisha madawa na vifaa tiba hapa nchini ili kwenda sambamba na malengo ya taifa ya maendeleo endelevu.
Akizungumzia kuhusu changamoto za bajeti kwenye eneo la Viwanda, muwasilisha mada Profesa Prosper H. Ngowi kutoka Chuo Kikuu Cha Mzumbe kampasi ya Dar es Salaam, alisema, fedha zilizotengwa kwenye Sekta ya Viwanda ni Shilingi Bilioni 81, 871,992,000, ambapo asilimia 51 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na asilimia 49 ni kwa ajili ya miradi ya maendeleo.
Kwa mtazamo wake, Profesa Ngowi alisema, mgawanyo huo ni mzuri na sio kwa kiwango kikubwa kwani hakuna tofauti na bajeti ya mwaka 2015/2016, na kuonyesha wasiwasi wake muda ambao Serikali inatoa fedha hizo kuhudumia maeneo yaliyokusudiwa.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu Kishiriki Cha Afya na Sayansi Shirikishi (MUHAS), Cha Muhimbili, Profesa Phares Mujinja, akitoa mada juu ya changamoto zinazoikabili bajeti ya Serikali ya 2016/2017 kwenye Sekta ya Afya wakati wa mdahalo huo.
“Bajeti ya 2016/2017 ni Asilimia 70.3% ya ile ya 2015/2016 na kwamba wizara hivi sasa ni kubwa kutokana na kuongezeka kwa sekta ya Uwekezaji.” Alifafanua. (P.T)

WAZIRI NAPE AONGOZA KUAGA MWILI WA MPIGAPICHA MKONGWE JOSEPH SENGA, JIJINI DAR

No comments:


 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye ambaye pia ni Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC), Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye jana ameongoza kuuaga mwili wa Mpigapicha Mkuu wa Tanzania Daina, Joseph Senga (pichani), ambaye ni mpigapicha mkongwe, aliyefariki dunia nchini India alikokuwa akipatiwa matibabu. Mwili wa Josefu Senga uliwasili nchini jana, na kuagwa jana, Sinza jijini Dar es Salaam, kwa ajili ya kusafirishwa kwenda kuzikwa nyumbani kwao mkoani Shinyanga.

 Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo Nape Nnauye akitoa heshima kwenye mwili wa marehemu Joseph Senga, Sinza jijini Dar es Salaam, jana
 Naibu Wazri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Anastazia wambura akitoa heshima kwa mwili wa Marehemu Joseph Senga jana Sinza Jijini Dar es Salaam
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe ambaye pia ni mmiliki wa Kampuni ya Free Media wachapishaji wa gazeti la Tanzania taima alilokuwa akifanyia kazi Joseph Senga, akitoa heshima mwa mwili wa marahemu Joseph Senga. Wafuatao ni waombolezaji wengine wakitoa heshima kwa mwili wa marehemu Joseph Senga
 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger