TRA

TRA

Wednesday, November 30, 2016

KIGOMA MJINI WAMPONGEZA LUKUVI KUTATUA MIGOGORO YAO YA ARDHI

No comments:


Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Willim Lukuvi anaendelea na ziara ya siku tatu katika mkoa wa Kigoma ambapo amefungua rasmi Baraza la Ardhi na Nyumba la Mkoa wa Kigoma pamoja na kutatua migogoro ya ardhi ya wananchi wa Kigoma. 

Wananchi hao wamempongeza Mhe. Waziri kwa hatua anazozichukua katika kumaliza migogoro yao ya ardhi na kuwajengea Baraza la Ardhi na Nyumba ambalo jipya na lililo na viwango kushinda mengine yote hapa nchini.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Willim Lukuvi akifungua Baraza la Ardhi na Nyumba la Mkoani Kigoma, Kushoto ni Mbunge wa Kigoma Mjini Mhe. Zitto Kabwe na kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe.Brigedia Jenerali Emanuel Maganga.
Jengo jipya la Baraza la Ardhi na Nyumba la Mkoani Kigoma.
Samani mpya za Baraza la Ardhi na Nyumba la Mkoani Kigoma.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Willim Lukuvi akiongea na wananchi wa Kigoma Mjini na kutatua migogoro yao ya ardhi.
Wananchi wa Kigoma Mjini wakiwasilisha malalamiko yao ya migogoro ya ardhi kwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Willim Lukuvi ili yaweze kutatuliwa.
wananchi wa Kigoma mjini wakimsikiliza Waziri wa Ardhi.

BODI YA UTALII NA ATCL WAINGIA MKATABA WA KUUTANGAZA UTALII WA NDANI

No comments:


Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii Nchini (TTB) Devotha Mdachi akikabidhiana mkataba  na Mkurugenzi wa ATCL Laislaus Matindi wakishuhudiwa na  Mwenyekiti wa TTB Jaji Mstaafu Thomas Mihayo pamoja na Mwenyekiti wa Shirika la ndege la ATCL, Mhandisi Emmanuel Korroso jana Jijini Dar es salaam. Chini wakiwa wanaweka saini ya makubaliano ya mkataba huo wakishuhidwa na mawakili wa pande zote mbili.


Mwenyekiti wa TTB Jaji Mstaafu Thomas Mihayo (Kulia)pamoja na Mwenyekiti wa Shirika la ndege la ATCL, Mhandisi Emmanuel Korroso  wakionesha vijarada vya Utalii vilivyozinduliwa jana Jijini Dar es salaam vitakavyokuwa vinapatikana katika ndege za Shirika la ATCL.

wakurugenzi kutoka shirika la ndege la ATCL na bodi ya Utalii TTB wakiwa wanafuatilia kwa makini mkutano huo.

Picha ya pamoja ya viongozi wa Shirika la Ndege la ATCL na Bodi ya Utalii TTB baada ya kumalizika kwa utiaji saini wa makubaliano ya mkataba wa pande hizo mbili.
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
BODI ya Utalii nchini (TTB) na Shirika la Ndege la Taifa (ATCL) limeingia mkataba wa pamoja leo Jijini Dar es salaam ikiwa ni lengo la kukuza soko la Utalii wa ndani na kuongeza pato la taifa nchini.
Akizungumza baada ya makabidhiano ya mkataba huo baina ya mkurugenzi wa TTB DevotAha Mdachi  na Mkurugenzi wa TTB  Laislaus Matindi, Mwenyekiti wa TTB, Jaji Mstaafu Thomas Mihayo amesema kuwa uwepo wa shirika la ndege la ATCL litasaidia katika ukuaji wa sekta ya utalii nchini kwani italeta chachu kwa watalii wa ndani na wa nje kuja kwenda kwa wingi.
Mihayo amesema kuwa TTB iliathirika kwa kiasi kikubwa sana hasa baada ya kutokuwepo kwa shirika la ndege na kutoa pongezi kwa juhudi zilizofanywa na Rais wa awamu ya Tano John Magufuli kwa kuirejesha upya na kuiwezesha kuwa na ndege zake zinazojiendesha zenyewe.
"Kwa juhudi zilizofanywa na Rais John Magufuli za kurejesha uhai kwa kampuni ya ATCL na kupata ndege zake ambazo zitasaidia kwenye kuutangaza utalii kwa watalii wa ndani na nje kwani itasaidia pia kuinua na kukuza pato ;la taifa kwa kuingiza fedha za kugeni,"amesema Mihayo.
Mkataba huo utakaowawezesha TTB kujitangaza Zaidi utawawezesha abiria watakaokuwa wanasafiri kwenda mikoa mbalimbali nchini kupata vipeperushi vilivyozinduliwa leo vinavyoelezea baadhi ya vivutio vya utalii pamoja na kuoneshwa kwa vituo hivyo kupitia TV za kwen ye ndege kuvionyesha.
Mwenyekiti wa Shirika la ndege la ATCL, Mhandisi Emmanuel Korroso amesema kuwa kwa safari za ndani katika mikoa mbalimbali, pia kwa sasa ATCL inataka kuongeza safari za ndege kwenda katika mikoa mingine.
Kuongezeka kwa safari hizo, pia kutachangia kwa watalii kutumia ndege za serikali na kusaidia kuinua uchumi wa nchi na utakuwa ni endelevu ili kuimarisha ushirikiano hiuo.(P.T)

ESRF YAFANIKISHA MKUTANO WA 5 WA MWAKA, WAJADILI UCHUMI

No comments:



Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dr. Ashatu Kijaji akihutubia katika mkutano wa tano wa mwaka wa ESRF wa kujadili sera za jamii na mahusiano yake kwenye mabadiliko ya kiuchumi nchini Tanzania ulioandaliwa na Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Jamii (ESRF) jijini Dar es Salaam.(Picha na Said Khalfan wa KVS Blog)
"Serikali inapofanya mipango inatakiwa kupanga mipango ambayo inajaribu kujibu kero za mwananchi, kama ni elimu, kama ni afyaa au kama ni kilimo cha kisasa, tunapotengeneza sera tuwe tunauwianisha, hizo sera zikitekelezeka na mteja wa bidhaa awe ameandaliwa ili mkulima asiwe amepoteza nguvu bure," alisema Luhanjo na kuongeza.
"Tunazungumzia nchi ya viwanda, viwanda gani? na nchi yetu niya kilimo kwahiyo tunatarajia viwanda vingi vitakuwa ni vya kilimo, kwahiyo tunataraji mkulima mdogo aimalishwe ili aweze kuzalisha mazao yanayokwenda kiwandani ni lazima sera ziwe na uwiano mzuri."
Nae Naibu Waziri wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji alisema Serikali inafahamu kuwa nchi haiwezi kupiga hatua bila kuhusisha mwananchi mmoja mmoja na inachofanya kwa sasa na kuwashawishi watu wenye viwanda kutumia malighafi ambazo zinazalishwa nchini ili wakulima nchini wafaidike na uwepo wa viwanda nchini.
"Tunaamini hatuwezi kuwa na uchumi unaokua kama hali ya kijamii ya wananchi haikui na hata Rais Magufuli alikuwa akisema tangu akiwa katika kampeni kwamba Tanzania ya Magufuli niya viwanda, na viwanda hivi ni kwa ajili ya watu wetu,

Mwenyekiti wa Bodi ya wadhamini wa ESRF, Philemon Luhanjo, akizungumza katika mkutano wa tano wa mwaka wa kujadili sera za jamii na mahusiano yake kwenye mabadiliko ya kiuchumi nchini Tanzania ulioandaliwa na ESRF.
"Kwenye mpango wetu wa miaka mitano tumesisitiza maendeleo ya viwanda lakini vinavyotumia malighafi zinazozalishwa hapa nchini katika kilimo chetu, kwahiyo hatuwezi kuwa na viwanda kama kilimo hakijaendelea, hatuwezi kuwa maendelo ya kijamii kama kilimo chetu hakijaendelea, kilimo ndiyo uti wa mgongo wa taifa letu, kwahiyo tumejadili hilo ili kuona wananchi wetu wananufaika vipi," alisema Kijaji.
Kwa upande wa Mkurugenzi Mtendaji wa ESRF, Dk. Tausi Kida alizungumza kuhusu mkutano huo ambao umedhaminiwa na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) na kusema,"ESRF kwasasa hivi tupo kwenye mchakato wa kutengeneza Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu ya mwaka 2017, "Katika hiyo ripoti tumeweza kutaharisha ripoti 11 ambazo zitachangia katika utayarishishaji wa hiyo ripoti na dhumuni kubwa ni kuweza kuzijadili hizo ripoti na kupata uelewa mpana ni kwa kiasi gani sera za kijamii zina mchango mkubwa katika kuleta mageuzi ya kiuchumi hapa Tanzania."

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Jamii (ESRF), Dk. Tausi Kida akitoa maelezo kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi katika mkutano huo.

Mkuu wa Programu, Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa UNDP, Amon Manyama akizungumza katika mkutano wa tano wa mwaka wa kujadili sera za jamii na mahusiano yake kwenye mabadiliko ya kiuchumi nchini Tanzania.(P.T)

UN NA EU YAWANOA MABALOZI 50 WA MALENGO YA DUNIA IRINGA

No comments:


Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akimkabidhi Ripoti ya Umoja wa Mataifa ya mpango wa misaada ya maendeleo UNDAP II 2016-2021 Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ruaha (RUCU) Iringa, Dr. Cephas Mgimwa alipomtembelea ofisini kwake mjini Iringa.
UMOJA wa Ulaya (EU) na Umoja wa Mataifa (UN) wameweka nguvu ya pamoja kuendesha kampeni ya uelewa wa malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) nchini Tanzania. Wakiwa Mkoani Iringa wamepata nafasi ya kuzungumza na wanachuo 1,000 kutoka vyuo vikuu vya Iringa na Ruaha kwenye semina iliyoelezea malengo ya dunia ambayo ni sehemu ya ajenda 2030 ya maendeleo endelevu duniani ambapo kati ya hao, vijana 50 wamepata semina ya mwongozo wa kuwa mabalozi wa malengo hayo (Global Goals Champions).
Kampeni hiyo imelenga kuwafanya vijana waelewe malengo 17 ya dunia ambayo kwa sasa yana mwaka mmoja tangu yapitishwe na kuwatanabaisha wajibu wao katika kufanikisha utekelezaji wake ndani ya mazingira ya Tanzania.

Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akifafanua jambo juu ya ripoti ya Umoja wa Mataifa ya Mpango wa misaada ya Maendeleo 2016-2021 (UNDAP II) kwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ruaha (RUCU) Iringa, Dr. Cephas Mgimwa alipomtembelea ofisini kwake mjini Iringa

Mwanasheria wa Chuo Kikuu cha Ruaha Iringa, Martin Noel akiwa ameongozana Mtaalam wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa nchini, Hoyce Temu kuelekea kwenye ukumbi wa mikutano chuoni hapo sambamba Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez aliyeambatana na Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro.

Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akiendesha semina ya malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) kwa vijana 50 kutoka Chuo Kikuu cha Iringa na Ruaha ambao watakuwa ni mabalozi wa malengo hayo ya dunia huku lengo la UN ni kuwaelimisha vijana zaidi ya 30,000 ifikapo mwaka ujao kuhusu malengo hayo ya dunia.

Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro akielezea fursa za ufadhili wa masomo nje ya nchi katika tovuti ya Umoja wa Ulaya Tanzania wakati wa semina ya malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) kwa vijana 50 kutoka Chuo Kikuu cha Iringa na Ruaha ambao watakuwa ni mabalozi wa malengo hayo ya dunia (Global Goals Champions) huku lengo la UN ni kuwaelimisha vijana zaidi ya 30,000 ifikapo mwaka ujao kuhusu malengo hayo ya dunia iliyofadhiliwa na EU.(P.T)

Tuesday, November 29, 2016

Magazeti ya Leo Jumatano

No comments:


 

Burundi yaishtumu Rwanda kwa kupanga kumuua msemaji wa rais Pierre Nkurunziza

No comments:


media
Willy Nyamitwe, akihojiwa na mwanahari wa RFI Kifaransa Sonia Rolley, hivi karibuni
Serikali ya Burundi, imeishtumu nchi jirani ya Rwanda kwa kupanga shambulizi dhidi ya msemaji wa rais Pierre Nkurunziza, Willy Nyamitwe.
Mmoja wa mlinzi wake aliuawa na mwingine kujeruhiwa katika shambulizi hilo huku Nyamitwe akijeruhiwa mkononi na kwenda kupata matibabu.
Katika ukurasa wake wa Twitter, Nyamitwe ameandika kuwa anaendelea vema lakini anaomboleza kifo cha mlinzi wake.
Msemaji wa Polisi nchini humo Pierre Nkurukiye, amesema watu waliokuwa wamejihami kwa silaha walipata maagizo kutoka Rwanda kumuua Nyamitwe.
Aidha, amesema baada ya shambulizi hilo wanajeshi wawili wa Burundi wamekamatwa kwa kuhusika katika shambulizi hilo lililotokea usiku wa kuamkia siku ya Jumanne.
Licha ya tuhma hizo, serikali ya Rwanda haijazungumzia tuhma hizo lakini imekuwa ikikanusha mara kwa mara kuhusika na machafuko nchini Burundi.
Uhusiano kati ya mataifa haya mawili umekuwa mbaya tangu jaribio la mapinduzi nchini Burundi mwaka 2015.
Burundi pia imekuwa ikiishtumu Rwanda kwa kuwapa mafunzo ya kijeshi wakimbizi wanaokimbilia katika nchi yake, ili kushambulia utawala wa rais Nkurunziza.RFI

Uteuzi wa Mwenyekiti na Makamu Mpya Azam FC

No comments:


father
ALIYEKUWA Makamu Mwenyekiti wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Nassor Idrissa (wa pili kutoka kulia kwenye picha), ameteuliwa kuwa Mwenyekiti mpya wa timu hiyo akirithi mikoba ya Alhaji Said Mohamed Abeid, aliyefariki dunia mwanzoni mwa mwezi huu.
Kwa mujibu wa barua iliyoandikwa na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Azam FC, Saad Kawemba, na kuituma kwenda kwenye Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kuwafahamisha mabadiliko hayo, imeeleza kuwa Shani Christoms Mligo, ndiye atakuwa Makamu Mwenyekiti mpya wa timu hiyo akichukua nafasi ya Idrissa.
Mabadiliko hayo ya kiuongozi yamefanywa na Bodi ya Wakurugenzi ya Azam FC, ambapo uteuzi huo umeanza rasmi jana Novemba 29 mwaka huu.(P.T)

NSSF YAENDELEA KUKAMILISHA MRADI WA JENGO LA MZIZIMA TOWERS

No comments:



Mkurugenzi wa Shirika la Hifadhi ya Jamii NSSF,Prof. Godius Kahyarara akizungumza na Waandishi kuhusiana na mradi wa Jengo la NSSF (Mzizima Tower) .
Baadhi ya Watumishi wa Shirika hilo wakiwa katika picha ya pamoja.
Na Anthony John blog Jamii.
Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii limekamilisha mradi wa Jengo refu Afrika Mashariki-Mzizima Tower lililopo barabara ya  Azikiwe na Mkwepu Dar es salaam.
Akizungumza na Waandishi wa Habari katika Makao Makuu ya Shirika hilo,Mkurugenzi wa Shirika hilo Prof. Godius Kahyarara  amesema Jengo hilo lipo hatua za mwisho za ukamilishaji wa ujenzi ambalo litakuwa na ghorofa 30 za makazi na 32 za Biashara.
Pia amesema Jengo hilo litakuwa na hoteli ya Nyota 5 na nyumba za makazi kwa ajili ya kuuza na kupangisha,Jengo linatarajiwa kukamilika mwakani 2017.Aidha Shilika hilo limesaini makubaliano na atakayekuwa muendeshaji wa Hoteli hiyo itakayokuwa katika Jengo la Mzizima na kutarajiwa kuanza kazi Mara moja baada ya Hoteli hiyo kufunguliwa.
"Baadhi ya miladi imekamilika na mengine ipo katika hatua za ukamilishwaji,NSSF inafungua rasmii upangishwaji wa litakalo kuwa Jengo refu Afrika Mashariki Mzizima Touwers" hayo amesema Kahyarara.(P.T)

BODI YA UTALII NA ATCL WAINGIA MKATABA WA KUUTANGAZA UTALII WA NDANI

No comments:



Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii Nchini (TTB) Devotha Mdachi akikabidhiana mkataba  na Mkurugenzi wa ATCL Laislaus Matindi wakishuhudiwa na  Mwenyekiti wa TTB Jaji Mstaafu Thomas Mihayo pamoja na Mwenyekiti wa Shirika la ndege la ATCL, Mhandisi Emmanuel Korroso jana Jijini Dar es salaam. Chini wakiwa wanaweka saini ya makubaliano ya mkataba huo wakishuhidwa na mawakili wa pande zote mbili.


Mwenyekiti wa TTB Jaji Mstaafu Thomas Mihayo (Kulia)pamoja na Mwenyekiti wa Shirika la ndege la ATCL, Mhandisi Emmanuel Korroso  wakionesha vijarada vya Utalii vilivyozinduliwa jana Jijini Dar es salaam vitakavyokuwa vinapatikana katika ndege za Shirika la ATCL.

wakurugenzi kutoka shirika la ndege la ATCL na bodi ya Utalii TTB wakiwa wanafuatilia kwa makini mkutano huo.

Picha ya pamoja ya viongozi wa Shirika la Ndege la ATCL na Bodi ya Utalii TTB baada ya kumalizika kwa utiaji saini wa makubaliano ya mkataba wa pande hizo mbili.
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
BODI ya Utalii nchini (TTB) na Shirika la Ndege la Taifa (ATCL) limeingia mkataba wa pamoja leo Jijini Dar es salaam ikiwa ni lengo la kukuza soko la Utalii wa ndani na kuongeza pato la taifa nchini.
Akizungumza baada ya makabidhiano ya mkataba huo baina ya mkurugenzi wa TTB DevotAha Mdachi  na Mkurugenzi wa TTB  Laislaus Matindi, Mwenyekiti wa TTB, Jaji Mstaafu Thomas Mihayo amesema kuwa uwepo wa shirika la ndege la ATCL litasaidia katika ukuaji wa sekta ya utalii nchini kwani italeta chachu kwa watalii wa ndani na wa nje kuja kwenda kwa wingi.
Mihayo amesema kuwa TTB iliathirika kwa kiasi kikubwa sana hasa baada ya kutokuwepo kwa shirika la ndege na kutoa pongezi kwa juhudi zilizofanywa na Rais wa awamu ya Tano John Magufuli kwa kuirejesha upya na kuiwezesha kuwa na ndege zake zinazojiendesha zenyewe.
"Kwa juhudi zilizofanywa na Rais John Magufuli za kurejesha uhai kwa kampuni ya ATCL na kupata ndege zake ambazo zitasaidia kwenye kuutangaza utalii kwa watalii wa ndani na nje kwani itasaidia pia kuinua na kukuza pato ;la taifa kwa kuingiza fedha za kugeni,"amesema Mihayo.
Mkataba huo utakaowawezesha TTB kujitangaza Zaidi utawawezesha abiria watakaokuwa wanasafiri kwenda mikoa mbalimbali nchini kupata vipeperushi vilivyozinduliwa leo vinavyoelezea baadhi ya vivutio vya utalii pamoja na kuoneshwa kwa vituo hivyo kupitia TV za kwen ye ndege kuvionyesha.
Mwenyekiti wa Shirika la ndege la ATCL, Mhandisi Emmanuel Korroso amesema kuwa kwa safari za ndani katika mikoa mbalimbali, pia kwa sasa ATCL inataka kuongeza safari za ndege kwenda katika mikoa mingine.
Kuongezeka kwa safari hizo, pia kutachangia kwa watalii kutumia ndege za serikali na kusaidia kuinua uchumi wa nchi na utakuwa ni endelevu ili kuimarisha ushirikiano hiuo.(P.T)

UN NA EU YAWANOA MABALOZI 50 WA MALENGO YA DUNIA IRINGA

No comments:


UMOJA wa Ulaya (EU) na Umoja wa Mataifa (UN) wameweka nguvu ya pamoja kuendesha kampeni ya uelewa wa malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) nchini Tanzania. Wakiwa Mkoani Iringa wamepata nafasi ya kuzungumza na wanachuo 1,000 kutoka vyuo vikuu vya Iringa na Ruaha kwenye semina iliyoelezea malengo ya dunia ambayo ni sehemu ya ajenda 2030 ya maendeleo endelevu duniani ambapo kati ya hao, vijana 50 wamepata semina ya mwongozo wa kuwa mabalozi wa malengo hayo (Global Goals Champions). Kampeni hiyo imelenga kuwafanya vijana waelewe malengo 17 ya dunia ambayo kwa sasa yana mwaka mmoja tangu yapitishwe na kuwatanabaisha wajibu wao katika kufanikisha utekelezaji wake ndani ya mazingira ya Tanzania. 

Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akimkabidhi Ripoti ya Umoja wa Mataifa ya mpango wa misaada ya maendeleo UNDAP II 2016-2021 Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ruaha (RUCU) Iringa, Dr. Cephas Mgimwa alipomtembelea ofisini kwake mjini Iringa.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akifafanua jambo juu ya ripoti ya Umoja wa Mataifa ya Mpango wa misaada ya Maendeleo 2016-2021 (UNDAP II) kwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ruaha (RUCU) Iringa, Dr. Cephas Mgimwa alipomtembelea ofisini kwake mjini Iringa
Mwanasheria wa Chuo Kikuu cha Ruaha Iringa, Martin Noel akiwa ameongozana Mtaalam wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa nchini, Hoyce Temu kuelekea kwenye ukumbi wa mikutano chuoni hapo sambamba Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez aliyeambatana na Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akiendesha semina ya malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) kwa vijana 50 kutoka Chuo Kikuu cha Iringa na Ruaha ambao watakuwa ni mabalozi wa malengo hayo ya dunia huku lengo la UN ni kuwaelimisha vijana zaidi ya 30,000 ifikapo mwaka ujao kuhusu malengo hayo ya dunia.

Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro akielezea fursa za ufadhili wa masomo nje ya nchi katika tovuti ya Umoja wa Ulaya Tanzania wakati wa semina ya malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) kwa vijana 50 kutoka Chuo Kikuu cha Iringa na Ruaha ambao watakuwa ni mabalozi wa malengo hayo ya dunia (Global Goals Champions) huku lengo la UN ni kuwaelimisha vijana zaidi ya 30,000 ifikapo mwaka ujao kuhusu malengo hayo ya dunia iliyofadhiliwa na EU.
Mkufunzi wa Malengo ya Dunia ambaye pia ni Mtaalam wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa nchini, Hoyce Temu akiwapiga msasa vijana 50 kutoka Chuo Kikuu cha Iringa na Ruaha ambao watakuwa ni mabalozi wa malengo hayo ya dunia (Global Goals Champions) huku lengo la UN ni kuwaelimisha vijana zaidi ya 30,000 ifikapo mwaka ujao kuhusu malengo hayo ya dunia kwenye semina hiyo iliyofadhiliwa na EU.
Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro akiwa amejumuika na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Iringa na Ruaha wakati wa semina ya malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) kwa vijana 50 ambao watakuwa ni mabalozi wa malengo hayo ya dunia (Global Goals Champions) huku lengo la UN ni kuwaelimisha vijana zaidi ya 30,000 ifikapo mwaka ujao kuhusu malengo hayo ya dunia ambapo semina hiyo imefadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU) nchini.
Pichani juu na chini ni vijana 50 kutoka Chuo Kikuu cha Iringa na Ruaha walioshiriki semina maalum ya kuwa mabalozi wa malengo ya dunia (Global Goals Champions) iliyoandaliwa na UN na kufadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU) mjini Iringa.
 
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez (kulia) akimkabidhi cheti Rais wa Chuo Kikuu cha Ruaha (RUCU) Iringa Athman Waziri aliyehitimu kuwa balozi wa Malengo ya Dunia (Global Goals Champion).
Picha juu na chini Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akiendelea na zoezi la kutunuku vyeti kwa mabalozi wa malengo ya dunia kutoka Chuo Kikuu cha Iringa na Ruaha.


Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez katika picha ya pamoja na Mabalozi wa Malengo ya Dunia (Global Goals Champions) baada ya kuhitimisha semina maalum iliyoshirikisha vijana 50 kutoka Chuo Kikuu cha Iringa na Ruaha.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez katika picha ya pamoja na Mwanasheria wa Chuo Kikuu cha Ruaha (RUCU) Iringa, Martin Noel baada ya kuhitimisha semina ya malengo ya dunia mjini Iringa.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez katika picha ya pamoja na Afisa Habari wa Chuo Kikuu cha Ruaha (RUCU), Muazarau Matola
Baadhi ya Global Goals Champions katika picha ya kumbukumbu na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez na Mtaalam wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa nchini, Hoyce Temu.
Mkufunzi wa Malengo ya Dunia ambaye pia ni Mtaalam wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa nchini, Hoyce Temu akibadilishana mawazo na wahitimu wa semina malengo ya dunia (Global Goals Champions) mara baada ya kuhitimisha semina hiyo iliyofanyika katika Chuo Kikuu cha Ruaha mjini Iringa ambapo imefadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU).
 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger