Muigizaji
wa Filamu nchini Tanzania, Shamsa Ford amefunguka kwa kuwaonya Mastaa
wa Wanawake waache tabia za kuchagua wanaume wa kuwaoa, kwani leo wana
majina makubwa na wanaonekana warembo lakini ipo siku itafika hata hao
wanaume wanaowatongoza leo watapotea kabisa.
Shamsa
Ford amesema kwa sasa Wanawake wenye majina makubwa wanajiona warembo
kiasi kwamba hufikia hatua hata ya kusubiri wanaume matajiri wa kuwaoa
bila kukumbuka kuwa hata hao matajiri wana watu wao huku wakisahau kuwa
ndoa ni baraka toka kwa Mungu na ina heshima kubwa sana.
“Wasichana
wenzangu maisha ni mafupi sana leo tunavuma na kupendwa kila kona
tunapokatiza ila kuna muda utafika hata nzi hakusogelei.Hata uwe mzuri
na maarufu kiasi gani lakini ndoa ina heshima yake.Msiwe wachaguzi
sana.Maana ukisema unamsubili tajiri aje akuoe na yeye huyo tajiri ana
mwanamke wake aliyetoka naye mbali kimaisha.“Ameandika Mrembo Shamsa Ford kwenye ukurasa wake wa Instagram huku akiwapa somo wanawake wenzie kuhusu Mwanaume wa kuoa
“Cha
muhimu ni kumuomba Mungu akupe mwanaume mwenye kumjua Mungu,mwenye
upendo,heshima,mtafutaji hayo mengine yanakuja tu..Nguvu ya mmoja ni
tofauti na ya wawili “Ameandika Shamsa Ford.
Shamsa Ford kwa sasa yupo kwenye ndoa na mfanyabiashara Chidi Mapenzi
SHARE









No comments:
Post a Comment