Katika
kuhakikisha madereva wanaosambaza bidhaa za kampuni wanafanya kazi zao
kwa ufanisi,kampuni ya TBL Group imeandaa mafunzo maalumu kwa madereva
kutoka viwanda vyake vilivyopo katika mikoa ya Dar es
Salaam,Arusha,Moshi,Mbeya na Mwanza.
Mafunzo
hao ambayo yamemalizikia mkoani Arusha yaliendeshwa na mkufunzi wa
madereva kutoka kampuni ya CFAO Motors,Hubert Kubo ambaye amewapatia
madereva hao elimu ya udereva wa kujihami ikiwemo utunzaji wa vifaa
wanavyoviendesha.
Baadhi ya
madereva waliohudhuria mafunzo hayo walishukuru mwajiri wao kwa
kuwapatia mafunzo mbalimbali kuhusiana na kazi yao ambayo walidai
yanawawezesha kufanya kazi yao kwa ufanisi na kuwa na uwezo wa kukabili
changamoto mbalimbali za kikazi kwa urahisi.
Madereva wakifuatilia mafunzo yaliyokuwa yanatolewa na Mkufunzi Hubert Kubo yaliyofanyika Arusha
Madereva wakifuatilia mafunzo yaliyokuwa yanatolewa na Mkufunzi Hubert Kubo yaliyofanyika Arusha
SHARE
No comments:
Post a Comment