Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa limetoa mwito kwa serikali ya 
Afghanistan kushughulikia kitisho kinachosababishwa na kundi la Taliban,
 al-Qaeda na makundi mengine yenye mafungamano na kundi la itikadi kali 
linaojiita Dola la Kiisilamu yanayotishia usalama na uthabiti wa nchi 
hiyo. Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limesisistiza juu ya 
kuendelea kuiunga mkono Afganistan katika suala la ulinzi na usalama 
ikiwa ni pamoja na juhudi za nchi hiyo za kupambana na ugaidi. Kundi la 
Taliban ambalo limekuwa likiendeleza uasi kwa zaidi ya miaka 15 dhidi ya
 serikali ya Afghanistan inayoungwa mkono na Marekani lilifanikiwa 
kudhibiti maeneo kadhaa nchini humo katika kipindi cha mwaka 2016 wakati
 vikosi vya Afghanistan vikijitahidi kupambana na wanamgambo hao tangu 
pale majeshi ya Marekani na yale ya NATO yalipohitimisha operesheni yao 
ya awali mwishoni mwa mwaka 2014.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)








No comments:
Post a Comment