• About
  • Services
  • Products
  • Blog
  • Contact Us

NCHI YANGU

Menu
  • Home
  • Lifestyle
    • Sub Menu 1
    • Sub Menu 2
    • Sub Menu 3
  • Sports
    • Sub Menu 1
      • Sub Menu 1
      • Sub Menu 2
      • Sub Menu 3
    • Sub Menu 2
    • Sub Menu 3
  • Post
  • Fitness
  • Music
  • Travel
  • Politics
  • Beauty

TRA

TRA

Monday, April 24, 2017

Home > > Uchaguzi Ufaransa: Emmanuel Macron na Marine Le Pen waongoza duru ya kwanza

Uchaguzi Ufaransa: Emmanuel Macron na Marine Le Pen waongoza duru ya kwanza

at 2:27 AM
Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !

Mgombea urais nchini Ufaransa Emmanuel Macron ameshinda duru ya kwanza ya uchaguzi wa nchi hiyo, huku dalili zikionyesha, baada ya wiki mbili atapambana katika duru ya pili na Marine le Pen ambae ni mgombea wa chama chenye mrengo wa kulia cha National Front. Aboubakar Famau na taarifa zaidi:

Macron mwenye umri wa miaka thelathini na tisa na aliyewahi kuwekeza katika sekta ya benki, hajawahi kuingia katika kinyang'anyiro cha uchaguzi kabla, amesema, shaka, hofu na hamu ya mabadiliko aliyokumbana nayo katika kampeni ndio iliyosababisha wapiga kura kuacha vyama vikuu vya kisiasa ambavyo vimekuwepo uongozini kwa miaka thelathini.




                                      Emmanuel Macron
"Nimesikia katika miezi iliyopita na leo tena, shaka, hasira na uoga waliokuwa nao wafaransa. Na hamu ya mabadiliko. Hiki ndicho kilichowasukuma kuacha vyama vikuu viwili vilivyotawala kwa zaidi ya miaka thelathini.")
Ameongeza kusema kazi yake hivi sasa ni kuipatanisha nchi na kuunganisha nguvu kwa ajili ya duru ya pili ya uchaguzi."wiki mbili kuanzia sasa, nataka niwe rais wenu. (CROWD CHEERING) Rais wa raia wote wa ufaransa. Rais wa wapenda nchi dhidi ya vitisho vya wanaotaka kujitenga.")
Kwa upande wake, Le Pen ameyaelezea matokeo hayo kuwa ni ya kihistoria. Huku akijiita kuwa yeye ni ndio chaguo la wafaransa na kusema kuwa muda umefika wa kuwabadilisha watu.
"Wakati umefika wa kuwaweka huru raia wa ufaransa na jamii yote wa rais wa Ufaransa bila kusahau marafiki zetu walio nje ambao wameniamini na naona fahari kwa imani walioonyesha kwangu.")
  • Uchaguzi Ufaransa 2017: Wanaowania ni akina nani?
Rais wa ufaransa amempigia simu bwana Macron na kumpongeza, bila kuonyesha kumuunga mkono rasmi.
 
                                      Wafuasi wa Bw Macron wakisherehekea...

Mmoja wa wasaidizi amesema haikuna vigumu kujua chaguo lake kati ya waziri aliyefanya kazi nae na mwakilishi mwenye mrengo wa kulia.Francois Fillon ambae ni mgombea wa mrengo wa kati, na aliyewahi kuwa waziri mkuu, ambae pia aliwahi kukabiliwa na tuhuma za ufisadi, wakati akiwahutubia wafuasi wake amesema atampigia kura Macron.
Wakati hayo yakijiri, kumetokea vurugu katikati mwa jiji la Paris zilizohusisha vijana wenye mrengo wa kushoto ambao hawakufurahishwa na ushindi wa Le Pen.
Polisi walipambana nao kwa kuwapiga viboko.Vile vile kumekuwa na maandamano magharibi mwa mji wa Nantes.
Tayari viongozi mbali mbali wa nchi za ulaya wameanza kuonyesha kumuunga mkono Macron.
Msemaji wa Chancellor wa ujerumani Angela Merkel amemtakia kila la heri, na kusifu msimamo wake kuunga mkono Umoja wa Ulaya.


                Wafuasi wa Marine Le Pen nao wakisherehekea
  
Hata hivyo, Le Pen pia amepata kuungwa mkono kutoka jamii ya kimataifa ambapo mwenyekiti wa kamati ya uhusiano wa mambo ya nje katika bunge la Urusi, amesema Le Pen ndio tegemeo pekee la mabadiliko.

Unknown

Author: Unknown

SHARE
  • Share
  • Tweet
  • Share
  • Pin
  • Share
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post
Fourni par Blogger CodeEnvoyer par emailBlogThis !Partager sur TwitterPartager sur FacebookPartager sur LinkedInÉpingler sur PinterestPartager sur StumbleUponVoter pour cet article sur HelloCoton

No comments:

Post a Comment

Newer Post Older Post Home
Subscribe to: Post Comments (Atom)

Tupate kupitia Facebook

Popular Posts

  • MKUU WA MKOA MARA WAANDISHI MKO SALAMA FANYENI KAZI KWA WELEDI.
    Mkuu wa Mkoa wa Mara Dkt Charles Mlingwa akiongea na waanadishi wa Habari Mkoa wa Mara katika maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyom...
  • Njiwa aliyetumiwa kusafirisha mihadarati
      Maafisa waligundua ...
  • MAGHEMBE APONGEZA OPERESHENI YA KUONDOA MIFUGO HIFADHINI MKOANI KAGERA
    Waziri wa Maliasili, Prof. Jumanne Maghembe (wa pili kushoto) akisalimiana na Viongozi wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa...

Popular Posts

  • MKUU WA MKOA MARA WAANDISHI MKO SALAMA FANYENI KAZI KWA WELEDI.
    MKUU WA MKOA MARA WAANDISHI MKO SALAMA FANYENI KAZI KWA WELEDI.
    Mkuu wa Mkoa wa Mara Dkt Charles Mlingwa akiongea na waanadishi wa Habari Mkoa wa Mara katika maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyom...
  • Njiwa aliyetumiwa kusafirisha mihadarati
    Njiwa aliyetumiwa kusafirisha mihadarati
      Maafisa waligundua ...
  • MAGHEMBE APONGEZA OPERESHENI YA KUONDOA MIFUGO HIFADHINI MKOANI KAGERA
    MAGHEMBE APONGEZA OPERESHENI YA KUONDOA MIFUGO HIFADHINI MKOANI KAGERA
    Waziri wa Maliasili, Prof. Jumanne Maghembe (wa pili kushoto) akisalimiana na Viongozi wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa...
  • FULL TIME: SERENGETI BOYS 3 vs 0 BURUNDI U-17
    FULL TIME: SERENGETI BOYS 3 vs 0 BURUNDI U-17
    Na Faustine Ruta, Bukoba Timu ya Vijana U17 ya Burudi leo kwenye uwanja wa Kaitaba imeanza mchezo wake wa kwanza wa kirafiki ...
  • Upasuaji wa kupandikiza kichwa unatarajiwa kufanyika kwa mara ya kwanza mwaka 2017
    Upasuaji wa kupandikiza kichwa unatarajiwa kufanyika kwa mara ya kwanza mwaka 2017
    DESEMBA  2017 inatarajiwa kuwa siku ya kihistoria kwenye sekta ya afya na tiba duniani ambapo utafanyika upas...
  • Rais wa Palestina akata mawasiliano na Israel
    Rais wa Palestina akata mawasiliano na Israel
      Rais wa Palestinia, Mahmoud Abbas amekata mawasiliano na serikali ya Israel hivyo kuzidisha mzozo ambao umekuwa ukitokota wiki nzima...

Pages

  • Home
  • About Us
  • Contat Us
 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger