TRA

TRA

Friday, May 19, 2017

Waziri wa zamani afaulu mtihani akiwa na miaka 82 India

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !

Waziri wa zamani ambaye anatumikia kifungo gerezaji baada ya kupatikana na kosa la kula rushwa amefaulu mtihani wa kumaliza shule India akiwa na miaka 82.

Om Prakash Chautala, aliyehudumu kama waziri mkuu wa jimbo la Haryana kaskazini mwa India kwa mihula minne, alifanya mtihani wa darasa la 12 akiwa katika jela ya Tihar mjini Delhi.

 Chautala alihudumu kama waziri mkuu wa jimbo la Haryana kaskazini mwa India kwa mihula minne

Mwanawe wa kiume Abhay Chautala alisema babake aliamua "kutumia vyema muda wake gerezani".
OP Chautala alipatikana na makosa kuhusiana na kuajiriwa kwa walimu.
Abhay Chautala aliambia gazeti la Indian Express kwamba babake amekuwa kila siku akienda kusoma katika maktaba ya gereza hilo.
"Husoma magazeti na vitabu. Huwa anawaomba wafanyakazi wa jela kumtafutia vitabu avipendavyo zaidi. Husoma vitabu kuhusu wanasiasa maarufu duniani,2 amesema.
Bw Chautala na 54 wengine, walipatikana na hatia ya kughushi vyeti walipokuwa wanwaajiri walimu 3,206 kati ya 1999 na 2000.
Waendeshaji mashtaka walisema watu waliokuwa wamehitimu zaidi walikataliwa na badala yake wale waliokuwa wametoa hongo wakaajiriwa.
Bw Chautala ni kiongozi wa chama cha Indian National Lok Dal Party na ni mwana wa aliyekuwa naibu waziri mkuu Devi Lal.

CHANZO: BBC

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger