TRA

TRA

Tuesday, July 18, 2017

HALI YA HATARI YATANGAZWA SUDAN KUSINI

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir ametangaza hali ya hatari kaskazini magharibi mwa nchi.

Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir ametangaza hali ya hatari kaskazini magharibi mwa nchi.

Taarifa iliyotangazwa na televisheni ya taifa haikutoa sababu ya kutangzwa kwa tahadhari hiyo.

Tahadhari hiyo inatarajiwa kusalia kwa kipindi cha miaka mitatu.
Mzozo wa Sudan Kusini umesababisha vifo vya maelfu ya watu na kuwalazimu wengine zaidi ya milioni mbili kuhama makwao tangu mwaka 2013.
Tahadhari ya kwanza ilitangazwa mwaka 2014 katika jimbo la Unity lililo kaskazini na lile la Jonglei lililo mashariki wakati waasi walipigana na vikosi vya serikali.

Msukosuko unashuhudiwa pande zote na mapigano yamesambaa hadi mashariki mwa nchi.

Umoja wa Matiafa unasema kuwa maelfu ya raia wamekimbia mji wa Pagak na maeneo yaliyo karibu, na kuvuka mpaka kuingia Ethiopia. Watoa misaada nao pia wamelazimika kuhama.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger