TRA

TRA

Friday, August 4, 2017

JUMBA LA PROFESA J KUBOMOLEWA

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !



SeeBait
Msanii wa muziki, ambaye ni Mbunge wa Mikumi kupitia CHADEMA, Joseph Haule maarufu kama Professa Jay nyumba yake ya kifahari aliyojenga pembezoni mwa barabara ya Morogoro maeneo ya Mbezi Luis, ipo hatarini kubomolewa kutokana na kuwa  miongoni mwa nyumba zilizowekewa alama ya X.

Nyumba za kifahari zilizojengwa pembezoni maeneo ya Kimara mpaka Kiluvya jijini Dar es salaam zimekumbwa na bomoabomoa kitu ambacho kimeumiza watu wengi sana, kwani wapo ambao hawana makazi na hawaelewi nyumba zao zikibomolewa wataanzia wapii na wataishi wapi.
Na nyumba ya Mbunge wa Mikumi ni moja ya nyumba ambazo zimewekewa X kuashiria nayo imo miongoni mwa nyumba za kubomolewa.
Hivi karibuni Tanroads imetangaza kuwa muda wowote itaanza utekelezaji wa kubomoa nyumba zilizowekewa alama ya X katika barabara hiyo kupisha ujenzi wa barabara kubwa ya kisasa.
Tayari Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limeanza kukata umeme kwenye nyumba nyingi hivyo kuwafanya baadhi ya wenye nyumba kubomoa wenyewe kwa hiari na kufungasha mizigo yao.
Tazama picha ya nyumba ya kifahari ya mbunge wa Chadema Joseph Haule maarufu kama Profesa jay ambaye hivi karibuni alifunga harusi kubwa na kuweka jiko ndani.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger