TRA

TRA

Monday, September 11, 2017

NAPE AZIDI KUFUNGUKA

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !
 
                                                  Mbunge wa jimbo la Mtama kupitia tiketi ya CCM, Nape Nnauye amefafanua kauli yake ya kuiunga mkono kauli ya Rais mstaafu,  Jakaya Kikwete na kuwataka viongozi waafrika waache kuwachukulia wapinzani wa vyama vya siasa kama maaduzi zao.

Akiongea katika mahojiano maalumu na Bongo5 wiki hii mkoani Dodoma, Nape amesema siasa isiwafanye watu wakaanza kuchukiana na kujengeana chiki. 
 
“Nilikomenti kupitia mitandao ya kijamii, nilisema mimi namuunga mkono  Jakaya. Wapinzani sio maadui, mimi nakaa nao napika nao chakula tunakula.
"Upinzani sio uadui, ni wadau katika kuendesha nchi, ndio maana mimi ishu ya Lissu nimepiga naye picha muda mchache kabla ya kupatwa na tukio, wapinzani wote mimi ni rafiki zangu na katika watu ambao wamefanya siasa za kupambana mimi ni mmoja wapo,” alisema Nape.

 Aliongeza, "wapinzani tuwachukulie kama ni washirika wetu, hakuna siku watatuunga mkono, lakini watatukosoa na tukiweka dhana hiyo hakuna siku tutawekeana vinyongo, halafu wakati mwingine sisi tunagombana wao wakubwa wanakaa meza moja wanakunywa chai, isifike mahali tukawekeana vinyongo tukataka kutoana roho, kwahiyo kimsingi namuunga mkono Kikwete na yeye aliendesha nchi kwa ustarabu huo, anakunywa nao chai, kwanini hakuwachukulia kama maadui.

"Yapo mambo Kikwete aliyafanya wakati wake hata sisi wakati mwingine ndani ya CCM tulikuwa tunachukia, unakuta mahali mmembana mtu halafu yeye anafika anasema muacheni, leo tunasema tulikuwa tunasikitika lakini nadhani alikuwa anafanya sawa si maadui zetu hawa,”

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger