Wanandoa wawili wenye asili ya India Jasbir mwenye
mika 67 na mkewe Bhupinder Kalsi mwenye miaka 61 pamoja na mtoto wao wa
kiume Devbir Kalsi mwenye umri wa miaka 33, wanashikiliwa na Polisi
Marekani baada ya wanandoa hao kusafiri kutoka India hadi Florida,
Marekani kwa lengo la kumpiga mke wa mtoto wao huyo kwa sababu si mtiifu
kwao.Mwanamke huyo anayeitwa Silky Gaind, 33, alipiga simu kwa wazazi wake walioko India na Polisi kuwajulisha kuwa amefungiwa ndani na anapigwa na mumewe na wakwe zake ndipo Polisi walipofika eneo hilo kumwokoa ambapo alikuwa anapigwa akiwa na mtoto wake.
Kwa mujibu wa Polisi walipofika eneo hilo walikuta mlango umefungwa na kuamua kuuvunja na walipoingia ndani waliwakuta watatu hao wakimshambulia mwanamke huyo huku taarifa zikieleza kuwa ni tabia ya mwanamme huyo kumpiga mkewe na wakati huu akaamua kuomba msaada wa wazazi wake.
SHARE








No comments:
Post a Comment