TRA

TRA

Friday, July 21, 2017

Majimarefu aomba kusaidiwa kukamilisha ujenzi wa madarasa

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !




Mwandishi Wetu, Korogwe

MBUNGE wa Korogwe Vijijini, Stephen Ngonyani 'Profesa Majimarefu' amemwomba Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Stella Manyanya kumwongezea nguvu ili kukamilisha ujenzi wa vyumba vya madarasa ya Sekondari ya Mazinde wilayani humo.
 Mbunge Korogwe Vijijini, Stephen Ngonyani

Majimarefu aliwasilisha ombi hilo kwenye mkutano wa hadhara uliohudhuriwa na mamia ya wananchi akitaka jamii kuungwa mkono katika kumalizia kazi ya ujenzi madarasa iliyoanza. 

Alisema wananchi kwa kushirikiana na mkuu wa wilaya hiyo wamefanya kazi kubwa kufanikisha ujenzi wa vyumba viwili, wakijitolea rasilimali zao ikiwemo nguvu kazi. 

Majimarefu alisema katika kuthamini mchango wa wananchi iko haja kwa Serikali kupitia wizara ya elimu kuunga mkono jitihada zilizoanza kuoneshwa kwenye eneo hilo. 

"Dada yangu,  Naibu Waziri Stella Manyanya, niseme kazi umeiona, sasa nikuombe najua utasema kitu hebu ona namna ya kutusaidia hapa," alisema. 

Licha ya kuyasema hayo, mbunge huyo alimmwagia sifa DC wa Korogwe, Robert Gabriel kwa utendaji kazi wake wenye ubunifu uliowezesha kutekelezwa miradi mbalimbali ya ujenzi yakiwemo madarasa. 

Gabriel alimhakikishia kiongozi huyo kuwa, fedha itakayolpelekwa kwa ajili ya miradi itakuwa salama na kutumika kama ilivyokusudiwa. 

Stella alisema wazazi wana jukumu la kuendelea kishirikiana na Serikali yao kufanikisha miradi mbalimbali ya maendeleo, hasa ujenzi wa madarasa. 

Alisema inasikitisha kuona wazazi wanashindwa kukarabati madarasa yaliyopo, huku wakimudu kuwapeleka watoto wao shule za kulipia, lakini kama wangekuwa na  ushirikiano mambo makubwa kwa maslahi ya jamii yangeweza kupatikana. 

Naibu Waziri huyo alikemea tabia za wazazi kuwaoza watoto wao na vitendo vya mimba dhidi ya watoto ambavyo huchangia kukwamisha vijana kutimiza ndoto za maisha. 

Akijibu maombi ya Profesa Majimarefu, Naibu waziri aliwaomba wananchi wa Mkomazi kuendelea kukamilisha kazi waliyoianza, huku akiahidi wizara kusaidia kukamilisha jitihada hizo. 

Alisema atahangaika huku na huko hadi kuhakikisha na kwamba atawawezesha wananchi wa Mazinde kujenga vyumba vingine viwili vya madarasa vitakavyoondoa changamoto iliyopo. 

ciao

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger