TRA

TRA

Monday, January 25, 2016

CRDB yatoa msaada wa viti Mbeya

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !
BENKI ya CRDB imetoa msaada wa viti 20 kwa ajili ya maabara ya Shule ya sekondari ya Kiwanja iliyopo wilayani Chunya Mkoa wa Mbeya.
 
 
Wakipokea msaada huo wakazi na wanafunzi wa shule ya sekondari ya Kiwanja  wameishukuru benki ya  CRDB  kwa kuwasaidia viti 20 kwa ajili ya chumba cha Maabara.
 
 
Akitoa msaada huo Meneja wa Benki hiyo tawi la Chunya Hamisi Mbinga alisema katika kutoa mchango kwa jamii wanayoizunguka na kuendeleza elimu waliamua kujitolea kwenye swala la maabara ili wanafunzi wa shule hiyo waweze kujifunza kwenye mazingira yaliyo bora.
 
 
Aliendeleza kueleza kuwa wao kama sehemu ya jamii wamekuwa wakishirikiana na wakazi wa chunya ambapo mbali na kutoa viti hivyo pia wameweza kuchangia kwenye sekta ya michezo kwa kutoa  kwa kiasi cha fedha cha shilingi laki nne.
 
 
Alisema laki mbili  zilikwenda Halmashauri kwa ajili ya kuchangia Michezo na laki mbili zilitumika katika ligi ya wilaya ambayo  ilikuwa ikijulikana kwa jina la kinawiro cup ambayo ilitumika kununua mipira.
 
 
Wakiongea kwa nyakati tofauti wakazi wa wilaya ya Chunya Jeremia Zakaria na Pasto Joshua walisema kwa kipindi kifupi toka tasisi hiyo ya crdb ianze kufanya huduma zake za kifedha  wilayani hapo wamekuwa wakishirikiana vizuri na benki hiyo kwa ukaribu kwenye maswala ya maendeleo na kufanya wilaya ya chunya izidi kukua kimaendeleo.
 
 
Mwisho. 

 

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger