TRA

TRA

Monday, January 25, 2016

Magufuli amng'oa Mkurugenzi Nida

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !
                             Dickson Maimu


RAIS Dk. John Magufuli ameendelea kutumbua majipu baada ya  kutengua uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida), Dickson Maimu pamoja na wasaidizi wake wanne.
Pia, ameagiza vyombo mbalimbali kufanya uchunguzi wa tuhuma zinazowakabili viongozi hao wa Nida.
Hayo yalisemwa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue wakati akizungumza na waandishi wa habari Ikulu jijini Dar es Salaam jana.
Balozi Sefue alisema Rais Magufuli amefikia uamuzi huo kutokana na taarifa za mamlaka hiyo kuonesha wamepokea fedha nyingi, lakini wameandikisha wananchi wachache kupata vitambulisho vya taifa.

 Alisema pamoja na Maimu, Rais ametungua pia uteuzi wa Mkurugenzi wa Teknolojia Habari na Mawasiliano (Tehama), Joseph Makani, Mkurugenzi wa Sheria, Sabrina Nyoni, Ofisa Ugavi Mkuu, Rahel Mapande na Ofisa Usafirishaji, George Ntalima.
Sefue alisema taarifa zilizomfikia Rais zinaonesha kuwa hadi sasa Nida imetumia sh. bilioni 179.6 kiasi ambacho ni kikubwa hivyo angependa kufanyike uchunguzi na ukaguzi ili kujua namna fedha hizo zilivyotumika.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger