Mkuu wa
Kitengo cha Mawasiliano na Huduma kwa Jamii, Susani Omari akizungumza na
Mameneja wa NHC na Wakurugenzi wakati wa zoezi la kupanda miti katika
Estate ya Kibada ikiwa ni jitihada za NHC kuboresha mazingira ya eneo
hilo linalokaliwa na wakazi takribani 1,000 katika nyumba zipatazo 218
za gharama nafuu. EMT wote(Directors, Regional Managers & Line
Managers) pia wametembelea miradi ya Kawe, Morocco Square, Victoria
Place, Eco Residence na Kibada ambako kumefanyika shughuli hiyo ya
upandaji miti.
Mkurugenzi
wa Rasilimali Watu wa Shirika la Nyumba la Taifa, James Rhombo akipanda
mti wa mchikichi katika eneo la makazi la NHC Kibada Kigamboni maarufu
kama Kigamboni Housing Estate.
Mwenyekiti
wa Chama cha Wafanyakazi (TAMICO), Lilian Reuben na Meneja wa NHC,
Mtwara, Joseph John wakipanda mti katika eneo la makazi la NHC Kibada
Kigamboni maarufu kama Kigamboni Housing Estate.
Zoezi la kupanda miti likiendelea katika eneo la makazi la NHC Kibada Kigamboni maarufu kama Kigamboni Housing Estate.(P.T)
Waziri wa
Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Hamad Rashid Mohammed ambae alikuwa
mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya Wakunga Duniani akibadilishana
mawazo na Mwenyekiti wa Baraza la Wauguzi na Wakunga Zanzibar Profesa
Amina Abdulkadr, (kulia) Waziri wa Afya Mahmoud Thabit Kombo na
(kushoto) Naibu Katibu Mkuu Wizara hiyo Halima Maulid Salum.
Mwenyekiti
wa Baraza la Wauguzi na Wakunga Zanzibar Profesa Amina Abdulkadr
akisoma risala ya wakunga katika maadhimisho ya siku ya Wakunga Duniani
yaliyofanyika Ukumbi wa Sanaa Rahaleo Mjini Zanzibar.
Mwakilishi
wa Shirika linaloshughulikia Idadi ya watu (UNFPA) akitoa salamu za
Shirika hilo kwenye maadhimisho ya siku ya Wakunga Duniani yaliyofanyika
Ukumbi wa Sanaa Rahaleo Mjini Zanzibar.
Waziri wa
Afya Mahmoud Thabit Kombo akimkaribisha Mgeni rasmi Waziri wa Kilimo,
Maliasili, Mifugo na Uvuvi Hamad Rashid Mohammed katika maadhimisho ya
siku ya Wakunga Duniani.(P.T)
SHARE








No comments:
Post a Comment