Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Prof. Justin Ntalikwa (mbele) akiongoza kikao cha uzinduzi wa Bodi ya Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Kaimu Kamishna wa Madini Nchini Mhandisi Ally Samaje akizungumza katika kikao cha uzinduzi wa Bodi ya Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) uliofanyika jijini Dar es Salaam
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia masuala ya madini Prof James Mdoe, akielezea historia ya Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) katika uzinduzi huo uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wajumbe wa Bodi Mpya ya Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) wakifuatilia kwa makini hotuba ya uzinduzi wa bodi hiyo iliyokuwa inatolewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Prof. Justin Ntalikwa.(hayupo pichani).
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Prof. Justin Ntalikwa (mbele kulia) akimkabidhi vitendea kazi Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) Balozi Alexander Muganda, (mbele kushoto) mara baada ya uzinduzi wa bodi hiyo uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Prof. Justin Ntalikwa (mbele kulia) akimkabidhi vitendea kazi mmoja wa wajumbe wa Bodi ya Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) Dk. Lightness Mzava, (mbele kushoto) mara baada ya uzinduzi wa bodi hiyo uliofanyika jijini Dar es Salaam
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Prof. Justin Ntalikwa ( wa tatu kutoka kushoto waliokaa mbele) Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia masuala ya madini Prof James Mdoe ( wa pili kutoka kushoto waliokaa mbele) wakiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Bodi ya Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) mara baada ya kumalizika kwa uzinduzi huo.
……………………………………………………………………………
Na Greyson Mwase, Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Prof. Justin Ntalikwa amezindua bodi ya wakurugenzi ya Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) na kuitaka bodi hiyo kuhakikisha kuwa shirika hilo linaendeshwa kibiashara na kuchangia katika ukuaji wa sekta ya madini.
Bodi hiyo iliyoteuliwa hivi karibuni na Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo inaundwa na wajumbe watano ambao ni pamoja na Abdalah Musa, Dkt. Coretha Komba, Felix Maagi, Dkt. Lightness Mnzava, John Seka chini ya Mwenyekiti wake Balozi Alexander Muganda.
No comments:
Post a Comment