TRA

TRA

Thursday, June 2, 2016

PROF NTALIKWA AZINDUA BODI YA STAMICO AITAKA KUHAKIKISHA STAMICO INAENDESHWA KWA FAIDA

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !
sta1Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Prof. Justin Ntalikwa (mbele) akiongoza kikao cha uzinduzi wa Bodi ya Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) uliofanyika jijini Dar es Salaam.
sta2Kaimu Kamishna wa Madini Nchini Mhandisi Ally Samaje akizungumza katika kikao cha uzinduzi wa Bodi ya Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) uliofanyika jijini Dar es Salaam
sta3Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia masuala ya madini Prof James Mdoe, akielezea historia ya Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) katika uzinduzi huo uliofanyika jijini Dar es Salaam.
sta4Baadhi ya wajumbe wa Bodi Mpya ya Shirika la Madini la  Taifa (STAMICO)  wakifuatilia kwa makini hotuba ya  uzinduzi  wa bodi  hiyo iliyokuwa inatolewa na Katibu Mkuu wa Wizara  ya Nishati na Madini Prof. Justin Ntalikwa.(hayupo pichani).
sta5Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Prof. Justin Ntalikwa (mbele kulia) akimkabidhi vitendea kazi Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Madini la Taifa (STAMICO)   Balozi Alexander Muganda, (mbele kushoto) mara baada ya uzinduzi wa bodi hiyo  uliofanyika jijini Dar es Salaam.
sta6Katibu Mkuu wa Wizara  ya Nishati na Madini Prof. Justin Ntalikwa (mbele kulia) akimkabidhi vitendea kazi mmoja wa wajumbe wa  Bodi ya  Shirika la Madini la  Taifa (STAMICO)   Dk. Lightness Mzava, (mbele kushoto) mara baada ya uzinduzi wa bodi hiyo  uliofanyika jijini Dar es Salaam
sta7Katibu Mkuu wa Wizara  ya Nishati na Madini Prof. Justin Ntalikwa ( wa tatu kutoka kushoto waliokaa mbele) Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya  Nishati na Madini anayeshughulikia masuala ya madini  Prof James Mdoe ( wa pili kutoka kushoto waliokaa mbele)  wakiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Bodi ya  Shirika la Madini la  Taifa (STAMICO) mara baada ya kumalizika kwa uzinduzi  huo.
……………………………………………………………………………
Na Greyson Mwase, Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Prof. Justin Ntalikwa amezindua bodi  ya wakurugenzi ya  Shirika la Madini la  Taifa (STAMICO) na kuitaka  bodi hiyo kuhakikisha kuwa shirika hilo linaendeshwa kibiashara na kuchangia katika ukuaji wa sekta ya madini.
Bodi hiyo iliyoteuliwa hivi karibuni na  Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo  inaundwa na wajumbe watano ambao ni pamoja na Abdalah  Musa, Dkt. Coretha Komba, Felix  Maagi, Dkt. Lightness Mnzava, John  Seka chini ya Mwenyekiti wake  Balozi  Alexander Muganda.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger