TRA

TRA

Sunday, June 26, 2016

Wakimbizi 50,000 wa kisomali kuondoka Dadaab

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


Kambi ya wakimbizi ya Dadaab nchini Kenya
Shirika la kuhudumia wakimbizi nchini Kenya limesema wakimbizi 50,000 wa kisomali wanaoishi kwenye kambi ya wakimbizi ya Dadaab watarejea makwao kwa hiyari mwishoni mwa mwaka huu.
Shirika hilo limesema kila mkimbizi atakayerejea atapatiwa dola za marekani mia mbili pia msaada wa chakula na matibabu kwa kipindi cha mpaka miezi tisa.
Mamlaka za Kenya zimesema zinataka kufunga kambi, hasa ambazo zinawatunza wasomali.
Mamlaka hizo zimesema zitawahamisha wakimbizi wa kutoka Sudani Kusini na kuwapeleka kwenye Kambi nyingine.
Idadi ya wakimbizi kambini Dadaab huenda ikapungua mpaka kufikia watu laki moja na nusu mwishoni mwa mwaka.BBC

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger