TRA

TRA

Saturday, July 2, 2016

OFISI YA MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA YAENDELEA NA UHAKIKI WA VYAMA NCHINI

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !



C1
Mhasibu kutoka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Bw.Willium Brown Nyamtiga akisisitiza jambo kwa viongozi wa Chama cha Alliance for Democratic Change (ADC) Jana wakati wa Zoezi la uhakiki uliofanyika katika ofisi za chama hicho zilizopo Jijini  Buguruni Dar es salaam .
Zoezi la uhakiki wa  utekelezaji wa masharti ya usajili wa Vyama va Siasa  kwa upande wa Tanzania Bara  linaendelea .Tayari  vyama 18 vimekwishakuhakikiwa. Vyama vinne vinatarajiwa  kuhakikiwa  Julai 4. Zoezi hili ni zoezi la kawaida na endelevu  ambalo hufanyika  kila mwaka ili kupima endapo vyama vya siasa   vinakidhi matakwa ya  Sheria ya usajili wa vyama vya Siasa.
Uhakiki wa Vyama vya siasa ni zoezi muhimu sana kwa sababu ni zoezi ambalo hugusa uhai wa  kila  chama cha siasa.  Kwa upande wa Tanzania Visiwani , uhakiki unatarajiwa kuanza  mara baada ya kumalizika Bara  kwa tarehe ambazo zitatangazwa baadaye.
C2
Bw.Eugene Kabendera, Katibu Mwenezi Taifa wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) akitoa taarifa  wa watumishi  kutoka Ofisi ya Msajili wa vyama vya Siasa wakati wa Zoezi la uhakiki uliofanyika katika ofisi za chama hicho zilizopo Jijini Makumbusho Dar es salaam Juzi
C3
Kaimu Katibu Mkuu wa Chama cha Jahazi Asilia, Bw. Mbwana S. Kibanda akifafanua jambo wakati wa zoezi la uhakiki  liliofanyika  Leo katika ofisi za chama hicho zilizopo ilala Jijini Dar es salaam. Kulia ni Mwenyekiti wa chama hicho na kushoto ni watumishi kutoka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa. (P.T)

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger