Kiti cha ubunge cha Atlanta katika jimbo hilo kilibaki wazi baada ya mbunge Tom Price kujiuzulu na kujiunga na serikali ya Trump.
Kuna wagombea 18, wakiwemo 11 wa Republican jambo ambalo linatishia kugawanya kura za chama hicho cha Rais Donald Trump.
Rais Donald Trump ameonekana kufuatilia uchaguzi huo na mara kadha ameandika kwenye Twitter akiwahimiza wanachama wa Republican kujitokeza kwa wingi kupiga kura.
Wilaya hiyo ya Atlanta imewakilishwa na wanasiasa wa Republican tangu mwaka 1979, lakini wakati huu wapinzani wao wana nafasi nzuri.
Chama cha Republican kilinusurika aibu wiki iliyopita baada ya kufanikiwa kutetea ubunge katika jimbo la kihafidhina Kansas, wadhifa ulioachwa wazi na Mike Pompeo aliyeteuliwa na Trump kuongoza CIA.
Uchaguzi utafanyika vipi?
Kuna wagombea 18, wakiwemo 11 wa Republican na watano wa Democratic.
Ikitokea kukosekane mgombea atakayepata zaidi ya asilimia 50 ya kura, wawili walioongoza watashiriki uchaguzi wa marudio tarehe 20 Juni.
SHARE









No comments:
Post a Comment