·
Wateja wa mtandao wa simu Zantel sasa
kufurahia mawasiliano na ndugu jamaa na marafiki waliopo mashariki ya kati kwa bei nafuu kwa kutumia
vifurushi cha kimataifa cha uarabuni.
Tunapokaribia
mwezi mtukufu wa Ramadhani, kampuni ya mtandao wa simu ya Zantel inaendelea kutimiza
ahadi yake ya kuongeza thamani katika maisha ya wateja wao na sasa kutangaza
ofa maalum inayowalenga waumini wa dini ya Kiislamu nchini wanapoelekea kuadhimisha mwezi mtukufu wa
mfungo wa Ramadhani duniani kote.
Akitangaza
habari hii makao makuu ya kampuni ya Zantel yaliyopo Msasani jijini Dar es
salaam Mkurugenzi mkuu wa Zantel Bwn. Benoit Janin amesema “Ramadhani ni muda
muafaka wa kujenga mahusiano mazuri na ndugu, jamaa na marafiki na ofa hii ni
ishara ya Zantel kuwasaidia wateja wake kuweza kuungana na kuwasiliana kwa urahisi zaidi na wapendwa
wao”.
Bwn. Janin ameelezea kwamba kutakua
na bidhaa mbalimbali zitakazotolewa katika kipindi hiki na anawasihi wateja wa
Zantel wavipe kipaumbele bidhaa hizi. Ofa hizi zitaanza rasmi tarehe 26/5/2017.
Akielezea
Zaidi kuhusu ofa hii, Meneja wa bidhaa na mawasiliano Bi. Rukia Mtingwa amesema
“Ofa hii itashirikisha vifurushi vya Bonga na Mpakabasi ambapo wateja wa Zantel
watapata punguzo la asilimia 50 kupiga simu kuanzia saa 5usiku hadi saa 11
asubuhi na Zaidi wataweza kupata huduma zetu mpya tulizozindua hivi karibuni
kama ‘ZanteL Madrassa’ ambapo wateja wanaweza kupata mufunzo ya dini ya kiislamu
kama Quran, Hadith, duah, habari za bakwata, na huduma nyingine nyingi
zinazopatikana kupitia kupiga simu, ujumbe wa maneno na programu za simu”.
Bi.Mtingwa
aliongezea kuwa wateja wa Zantel wanaweza kuwapigia simu ndugu jamaa na
marafiki waliopo mashariki ya kati kwa bei nafuu zaidi kupitia kifurushi cha kimataifa cha uarabuni.
Kwa shilingi za kitanzania 2,000 wateja watapata dakika 4 za kupiga simu Qatar, Oman, UAE, Lebanon, Pakistan, Yemen
& Saudi Arabia, na kwa shilingi 5,000 watapata dakika 10 kupiga simu kwenda
kwenye nchi tajwa, na fedha hizi
zitakatwa moja kwa moja kwenye akaunti za salio za wateja.
Vifurushi
vyote hivi vitapatikana kwa kujiunga kwa kupiga *149*15# na kwa vifurushi vya
‘Bonga Mpakabasi’, ‘Zantel Madrassa’ wateja wataweza kujiunga kwa kutuma
ujumbe wa maneno kwa kutumia neno SUB na
kutuma kwenda namba 15586 au kwa kupiga namba 15586
Zantel
inaendelea na mradi wake wa kuboresha mtandao wake kuwa wa kisasa Zaidi
visiwani Zanzibar ili kuhakikisha wateja wake wanafurahia huduma zinazoaminika
Zaidi zikiwemo huduma ya mtandao wa intaneti wa kasi Zaidi wa 4G, na kwa mara
ya kwanza huduma za kibenki za KIISLAM kupitia simu za mkononi.
SHARE









No comments:
Post a Comment