TRA

TRA

Friday, June 23, 2017

Kamati ya Kudumu Bunge la Msumbiji yatembelea NEC

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !
 Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Tanzania (NEC) Jaji (R) Mhe. Semistocles Kaijage (kulia) akimkabidhi Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Utawala na Serikali za Mitaa ya Bunge la Msumbiji, Mhe. Lucas Chomera Jeremiah (kushoto) Ripoti ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania wa Rais, Wabunge na Madiwani mwaka 2015 wakati Kamati hiyo ilipotembelea Ofisi za Tume leo jijini Dar es salaam.


Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji (R) Mhe. Semistocles Kaijage (katikati) akitoa ufafanuzi kuhusu majukumu ya Tume kwa  Wabunge wa Bunge la Msumbiji ambao ni Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa waliotembelea Ofisi za NEC jijini Dar es salaam kujifunza namna Tume hiyo inavyotekeleza majukumu yake kwa mujibu wa Katiba. Kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Lucas Chomera Jeremiah na Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC Bw. Hamis Mkunga.




Mkurugenzi wa Huduma za Sheria wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Bw. Emmanuel Kawishe (kushoto) akiwaeleza Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Utawala na Serikali za Mitaa ya Bunge la Msumbiji namna Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Tanzania inavyotekeleza majukumu yake kwa mujibu wa Katiba.

 Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Utawala na Serikali za Mitaa ya Bunge la Msumbiji, Mhe. Lucas Chomera Jeremiah (kushoto) akifafanua jambo wakati wa kikao cha Wajumbe wa Kamati hiyo kutoka Msumbiji na watendaji wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Tanzania leo jijini Dar es salaam, Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Utawala na Serikali za Mitaa ya Bunge la Msumbiji wamezitembelea Ofisi za NEC kwa lengo la kujifunza na kubadilishana uzoefu katika masuala ya Uchaguzi.Kulia ni Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji (R) Semistocles Kaijage.

 Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Tanzania (NEC) Jaji (R) Mhe. Semistocles Kaijage (Kulia) akisalimiana na Wabunge wa Bunge la Msumbiji na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Utawala na Serikali za Mitaa wa nchi hiyo waliotembelea Ofisi za NEC kujifunza na kubadilishana uzoefu kuhusu uendeshaji wa chaguzi mbalimbali.

Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Tanzania (NEC) Jaji (R) Mhe. Semistocles Kaijage (wa tatu kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Utawala na Serikali za Mitaa ya Bunge la Msumbiji waliozitembelea Ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi leo jijini Dar es salaam.  PICHA/Aron Msigwa - NEC

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger