Tunapoelekea
kipindi hiki cha sikukuu ya Eid El Fitri, Jeshi la Polisi nchini, linatoa tahadhari kwa
wananchi kuwa makini katika suala zima la ulinzi na usalama wa maisha na mali zao. Kipindi kama hiki cha sikukuu baadhi ya watu
hupenda kutumia fursa hiyo kufanya vitendo vya uhalifu na vitendo vingine
ambavyo huhatarisha usalama wa watu na mali zao.
Hata hivyo, Jeshi
la Polisi nchini, limejipanga kwa
kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama katika mikoa yote
kuhakikisha kwamba wananchi
wanasherehekea Sikukuu katika hali ya amani
na utulivu.
Aidha, ulinzi
umeimarishwa kwenye maeneo yote, yakiwemo maeneo ya kuabudia, fukwe za bahari,
sehemu za starehe na maeneo mengine ambayo yatakuwa na mikusanyiko mikubwa ya
watu.
Vilevile, Jeshi la Polisi linawatahadharisha watumiaji
wa vyombo vya moto barabarani kuwa makini na kuzingatia sheria na kanuni za usalama
barabarani, Jeshi la Polisi halitasita
kuwachukulia hatua kwa wale wote watakaovunja
sheria na kanuni za usalama barabarani kwa mabereva kutumia vilevi,
bodaboda kubeba mishikaki, kwenda mwendo
kasi pamoja na kupiga honi hovyo.
Pia,
tunawataka wananchi wote kuwa wepesi
katika kutoa taarifa kwa kupitia namba za simu za bure 111 au 112 pindi wanapoona viashiria vyovyote vya
uhalifu katika maeneo yao ya makazi ama maeneo ya biashara.
Tunawatakia
watanzania wote Sikukuu njema ya Eid El Fitri.
Imetolewa na:
Advera John Bulimba -ACP
Msemaji wa Jeshi la Polisi.
Makao Makuu ya Jeshi la Polisi
SHARE









No comments:
Post a Comment