TRA

TRA

Friday, August 25, 2017

BARCELONA KUVUNJA TENA REKODI

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !

 

Barcelona wanakaribia kumfanya mchezaji wa Borussia Dortmund Ousmane Dembele mchezaji wa pili aliye ghali zaidi katika historia.

Boruissia Dortmund ilikataa ombi la Barcelona kumunua mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20 anayeaminika kuwa na thamani ya Yuro milioni 100, mapema mwezi Agosti huku mchezaji huyo akipigwa marufuku kwa kukosa kufika mazoezini.

Kitita hicho hatahivyo kinakadiriwa kuwa chini ya Yuro milioni 222 ambazo PSG iliilipa Barcelona kumnunua Neymar mnamo mwezi Agosti.


 Ousmane Dembele wa Borrusia Dortmund

Hathivyo kitita hicho kitakipiku kile kilichotolewa na Manchester United kumnunua Paul Pogba kutoka Juventus.

Mchezaji wa Ufaransa Dembele hajaichezea Dortmund tangu kombe la Supercup mnamo tarehe 5 Agosti.

Alijiunga na timu hiyo ya Bundesliga kutoka klabu ya Rennes kwa Yuro milioni 15 miezi 12 iliopita akiwa ameanza kucheza mwaka 2015.

CHANZO: BBC

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger