TRA

TRA

Thursday, August 3, 2017

Jumba refu laungua Dubai

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


                    Jumba refu la Torch Tower UAE

Moto mkubwa umeunguza mojawapo ya jumba refu duniani, Torch Tower huko Dubai UAE kwa mara ya pili katika kipindi cha miaka miwili.

Picha zilizowekwa katika mitandao ya kijamii zilionyesha moto huo ukisambaa hadi katika jumba hilo huku vifusi vilivyokuwa vikichomeka vikianguka.

Mamlaka baadaye ilisema kuwa wafanyikazi walifanikiwa kuwaondoa watu na wakafanikiwa kuudhibiti moto huo.
Haijulikani ni nini kilichosababisha moto huo katika mojawapo ya jumba refu duniani. 

Hakuna majeraha yoyote yalioripotiwa kufikia sasa katika jumba hilo la Torch Tower ,kulingana na mamlaka ya Dubai iliotuma ujumbe katika Twitter.

Jumba hilo la Torch Tower liliharibiwa na moto mwengine 2015.

CHANZO: BBC

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger