TRA

TRA

Thursday, August 3, 2017

Mwanamume aliyeingizwa kwenye jeneza Afrika Kusini atoa ushahidi Mahakamani

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !







Kisa hicho kilizua ghadhabu kubwa nchini Afrika Kusini.
Mwanamume mmoja mweusi ambaye anadaiwa kulazimishwa kuingia ndani ya jeneza na wanaume wawili wazungu ambao walitisha kumchoma akiwa hai ametoa ushahidi mbele ya mahakama nchini Afrika Kusini.

Victor Mlotshwa alingua kilio kwenye mahakama kuu ya Middleburg wakati alikumbuka kisa hicho cha mwezi Agosti mwaka uliopita.
Mahakama ilicheza video ya kisa hicho ambapo bwana Mlotshwa anaweza kusokika akilia na kuomba washambuliaji kumsamehe. 

Anadai kuwa wakulima Theo Jackson na Willem Oosthuizen walimfunga kwa nyaya wakampiga na kutishia kumpiga risasi.
Washukiwa hao wawili wanakana hilo wakidai kuwa walimpata bwana Mlotswa akiiba nyaya.
Wanasema kuwa lengi lao lilikuwa ni la kumfunza adabu. Kisa hicho kilizua ghadhabu kubwa nchini Afrika Kusini.

CHANZO: BBC

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger