Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya
Nishati na Madini, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo (mbele) akiongoza
kikao kilichoshirikisha watendaji kutoka Shirika la Umeme Tanzania
(TANESCO) Kanda ya Kusini na Ofisi za TANESCO mkoa wa Mtwara mjini
Mtwara
Sehemu ya watendaji kutoka
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Kanda ya Kusini na Ofisi za TANESCO-
Mtwara wakifuatilia maelekezo yaliyokuwa yanatolewa na Naibu Katibu
Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo
(hayupo pichani) katika kikao hicho.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo akisisitiza jambo katika kikao hicho
Afisa Rasilimaliwatu wa Kanda ya
Kusini, Bonus Msuha (kushoto) akieleza jambo katika kikao hicho. Kulia
ni Meneja wa TANESCO-Mtwara Mhandisi Aziz Salum
Sehemu ya watendaji kutoka
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Kanda ya Kusini na Ofisi za TANESCO-
Mtwara na Wizara ya Nishati na Madini wakifuatilia maelekezo
yaliyokuwa yanatolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na
Madini, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo (hayupo pichani) katika kikao
hicho.
……………………….
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya
Nishati na Madini, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo leo tarehe 24
Agosti, 2017 amefanya kikao cha kazi na watendaji wa Shirika la Umeme
Tanzania (TANESCO) Kanda ya Kusini na Ofisi za TANESCO mkoa wa Mtwara
mjini Mtwara lengo likiwa ni kujadili mafanikio na changamoto za
utendaji kazi. Dkt. Pallangyo amewataka watendaji hao kuwa wabunifu
kwenye ukusanyaji wa mapato pamoja na kuwasilisha taarifa za
utekelezaji za kila baada ya miezi mitatu.
SHARE








No comments:
Post a Comment