TRA

TRA

Wednesday, August 23, 2017

OFISA MTENDAJI MKUU WA STANDARD CHARTERED BANK-TANZANIA, AWAHAMASISHA WAFANYAKAZI WA AIRTEL

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !
 

Mfanyaakzi wa Airtel-Tanzania, akifuatilia kwa shauku yale yaliyokuwa yakizungumzwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa Standard Chartred Bank-Tanzania,  wakati wa semina ya "kuhamasisha" (Motivation), iliyowaleta pamoja wafanyakazi wa kampuni hiyo makao makuu wakiongozwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa Airtel, Bw. Sunil Colaso, leo Agosti 23, 2017

NA K-VIS BLOG/Khalfan Said
WAFANYAKAZI wa kampuni ya simu za mikononi, Airtel-Tanzania, wamehimizwa kuzingatia utendaji wa kazi wenye malengo na kutimiza malengo hayo bila kukata tama.
Hayo yamesemwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa Standard Chartered Bank-Tanzania, Bw.Anjay Rughani, (pichani), wakati akitoa mada kwenye semina ya kuhamasisha (motivation), wafanyakazi hao, makao makuu ya kampuni hiyo jijini Dar es Salaam leo Agosti 23, 2018.
“Mimi ni Mtanzania kutoka Mbeya, nimepitia mikiki mikiki mingi hadi kufikia hapa nilipo, na ningewaomba ndugu zangu, kila uamkapo fanya tathmini ya malengo uliyojiwekea ni kwa kiasi gani umefikia tena bila kuchoka” Alisema.
Bw.Rughani ni mmoja kati ya watanzania wawili ambao wanashika wadhifa mkubwa, (CEO), kwenye taasisi kubwa ya kifedha yenye nguvu kama Standard Chartered Bank. Mtanzania mwingine ni Dkt. Charles Kimei, ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, benki ambayo chini ya uongozi wake, imepiga hatua kubwa miongoni mwa taasisi kubwa za kifedha hapa nchini.
Hata ninyi hapa leo mnaweza kufikia hatua ambayo mimi nimefikia, kwani hakuna jambo linaloshindikana, muhimu ni kuweka malengo, kujielekeza kwenye malengo hayo na kujituma kwa kiwango cha juu na hatimaye utaona matokeo bora, alisisitiza.
 Lengo la semina hii ni kuhamasisha wafanyakazi wa kampuni ya Airtel, kuzingatia misingi ya utendaji kazi, kwa kujituma, ubunifu, kuweka malengo na kuyatekeleza hadi kuona matokeo yake, Afisa Mtendaji Mkuu wa Airtel-Tanzania Bw. Sunil Colaso, akliwaambia wafanyakazi hao wakati akimkaribisha Bw. Sunil kutoa “somo” hilo.
Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Airtel-Tanzania, Bw. Sunil Colaso, (kushoto), akimpongeza Bw. Rughani, baada ya kuwasilisha mada hiyo.

 Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Airtel-Tanzania, Bw. Sunil Colaso, akizungumza mwanzoni mwa semina hiyo.
 Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Airtel-Tanzania, Bw. Sunil Colaso, akizungumza mwanzoni mwa semina hiyo.
 Mfanyakazi wa Airtel- Tanzania, akizungumza wakati wa semina hiyo.
 Mfanyakazi wa Airtel- Tanzania, akizungumza wakati wa semina hiyo.

Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Airtel-Tanzania, Bw. Sunil Colaso, (kushoto), akibadilishana mawazo na Wakurugenzi kutoka kulia ni Isack Nchunda(Mkurugenzi wa Masoko, Frank Filman (Mkurugenzi wa IT), na Emmanuel Luanda, (Kaimu Mkurugenzi wa Mtandao-Network)

Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Airtel-Tanzania, Bw. Sunil Colaso, (kulia), akizungumza jambo na Afisa Mtendaji Mkuu, wa Standard Chartered Bank-Tanzania, Bw. Anjay Rughani
 Baadhi ya wafanyakazi waliohudhuria semina hiyo.
Wafnyakazi wakisikiliza kwa makini "somo" lililokuwa likitolewa na Bw. Rughani.
 Bw. Sanjay Rughani, na Bw. Sunil Colaso, wakiwa katika picha ya pamoja na watayarishaji w semina hiyo.

Afisa Mtendaji Mkuu, wa Standard Chartered Bank-Tanzania, Bw. Anjay Rughani, ambaye ni mmoja kati wa watanzania wachache wanaoshikilia nafasi hiyo ya juu kwenye taasisi za kimataifa, akizungumza wakati wa semina ya kuwahamasisha (motivation), wafanyakazi wa kampuni ya simu za mikononi, Airtel, makao makuu, jijini Dar es Salaam, Agosti 23, 2017.

Wafanyakazi wakisikiliza

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger