TRA

TRA

Wednesday, September 6, 2017

Misri waipiku Uganda Kombe la Dunia

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !

 

 
Misri walilipiza kisasi kichapo cha Ijumaa mikononi mwa Uganda mjini Kampala kwa kuwalaza 1-0 mjini Alexandria na kuongoza tena Kundi E Jumanne.

Mohamed Salah alifunga bao la ushindi dakika ya sita, jaribio lake la pili baada ya kipa wa Uganda Dennis Onyango kuzuia kombora lake la kwanza kuingia.

Onyango alifanya kazi ya ziada kuzuia Uganda kushindwa.
Kulikuwa na sherehe kubwa mwisho wa mechi hiyo miongoni mwa raia wa Misri, ambao hawajashiriki Kombe la Dunia tangu 1990 licha ya kushinda mataji manne ya Kombe la Taifa Bingwa Afrika tangu wakati huo.
 Mo Salah alifungia Misri bao pekee mechi hiyo dakika ya sita

Misri sasa wana alama tisa, Uganda saba nao Ghana - ambao walicheza fainali tatu zilizopita za Kombe la Dunia - wakiwa nafasi ya tatu na alama tano baada ya kulaza Jamhuri ya Congo 5-1 mjini Brazzaville. 

Congo, wana alama moja pekee, na hawawezi tena kufuzu kwa michuano hiyo itakayofanyika Urusi mwaka ujao.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger