TRA

TRA

Thursday, September 7, 2017

RAIS DKT.MAGUFULI AWASIMAMISHA KAZI MAWAZIRI,MAKATIBU WAKUU

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


PIC 2
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa  Dkt John Pombe Magufuli akizungumza mara baada ya kupokea ripoti  mbili za Kamati Maalum  za Bunge zilizofanya uchunguzi wa Biashara ya Madini ya Almasi na Tanzanite Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Jonas Kamaleki- MAELEZO
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli ameamuru wateule wake wote waliotajwa kuhusika na suala la upotevu wa madini ya Almasi na Tanzanite kukaa pembeni ili vyombo vya usalama vifanye kazi yake.
Mhe. Rais ameyasema hayo jana Ikulu, jijini Dar es Salaam wakati wa kupokea ripoti za Kamati za Bunge zilizochunguza madini ya Almasi na Tanzanite.
Amesema viongozi hao waliotajwa iwe ni Waziri, Katibu Mkuu, Katibu Tawala, Mkurugenzi au kiongozi yeyote aache kazi kwani Tanzania haiwezi kuendelea kuibiwa wakati viongozi hao wanaendelea kuwa serikalini.
Rais Magufuli amesema mapendekezo na yote yaliyoandikwa kwenye ripoti hizo mbili Serikali itayatekeleza kwa asilimia 100.
“Nchi yetu ni ya maajabu kweli, ajabu kubwa mojawapo ni kuwa hata hatujali raslimali zetu,”alisema Rais Magufuli.
Akionyesha kusikitishwa na upotevu wa raslimali hizo, Rais Magufuli amasema kuwa Tanzania imechezewa kwa kipindi kirefu na kuwafanya watanzania kuishi maisha magumu wakati wanaoibia nchi wakineemeka.
“Hao wanaotuchezea wanatuona sisi si binadamu au ni majitu tu, wangetuona kama binadamu wangetupa basi asilimia inayofaa,”alisema Magufuli.
Aidha, Rais Magufuli amewataka watanzania kuwa wazalendo kwa kujali na kuthamini mali na raslimali za umma ili kuondoa nchi katika utegemezi wakati nchi ina kila kitu cha kuifanya kuwa tajiri hadi kutoa misaada kwa nchi nyingine.
Ameagiza vyombo vya ulinzi na usalama kufuatilia mapendekezo na matokeo ya ripoti hizo kwa haraka ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa dhidi ya wahusika.
Katika kusisitiza utekelezaji wa hatua hizo, Rais Magufuli amekabidhi ripoti hizo mbili kwa Mkurugenzi wa TAKUKURU, Bwana Valentino Mlowola na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi  Jenerali Venus Mabeyo.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger