Watoto
2 Ikram na Maureen, kati 4 waliotekwa wamepatikana wakiwa wamefariki
dunia katika shimo la choo ambacho bado halijaanza kutumika.
Mwenyekiti
wa Mtaa wa Olkerian huko Olasiti jijini Arusha, Daudi Safari,
amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba Jeshi la Polisi limeopoa
miili ya watoto hao jana jioni.
Inadaiwa
kuwa mtekaji aliwatumbukiza ndani ya shimo hilo wakiwa hai kabla ya
kuondoka na kuelekea Geita ambapo amekamatwa na kusema walipo watoto
hao.
Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Geita, Mponjoli Mwabulambo amethibitisha taarifa za
kukamatwa kwa mtekaji huyo aliyetambuliwa kwa jina la Samson Petro
mwenye umri wa miaka 18.
Kamanda
Mwabulambo amesema kijana huyo alikamatwa katika nyumba ya kulala
wageni ya Shitungului iliyopo mji mdogo wa Katoro akiwa na mtoto mdogo
mwenye miaka miwili.
Alisema
mtuhumiwa alimficha mtoto huyo katika chumba namba 11 cha nyumba hiyo
ya kulala wageni wakati akisubiri mpango wake wa kutaka alipwe shilingi
milioni nne na wazazi wa mtoto huyo Ombeni Mshana na Elizabeth Ombeni.
SHARE









No comments:
Post a Comment