Na Anthony John Glob ya Jamii.
Mkuu
wa wilaya ya kinondoni Alli Hapi ametoa muda wa siku saba kwa wachimba
kokoto wa eneo la Boko chama kuondosha mawe yao yaliyopo kwenye eneo
hilo, ili kupisha ujenzi wa dampo la kisasa.
Kauli hiyo ya DC Hapi imekuja baada ya kutembelea na kukagua eneo hilo ambalo awali wachimbaji wake walipewa amri ya kutokuendelea na uchimbaji wa kokoto, lakini baadhi wamekaidi amri hiyo na kuendelea.
Akielezea zaidi Hapi amewataka kutokuendelea kuchimba na hasa katika kipindi hiki cha mvua, kwani wanaweza kujisababishia madhara ya kufukiwa na kifusi na kupoteza uhai.
Amesema amewaelekeza maafisa mazingira na mipango miji wa manispaa waunde timu ,waangalie uwezekano wa kuweka dampo kwenye eneo hilo, kwani eneo la dampo lililopo ni moja Pugu Kinyamwezi, ambako ni mbali.
Aidha amesema dampo hilo lifanywe la kisasa ili uwe mradi ambao utasaidia kuingiza mapato kwa manispaa.
Aidha HAPI ameeleza kuwa pindi eneo hilo litakapoanza kutengenezwa watu waliokuwa wakichimba hapo waandae orodha ya majina ili mawe yatakayotolewa hapo wapewe wao.
Kwa upande wake afisa mazingira wilaya ya kinondoni Mohamed Msangi amesema, eneo hilo likifanywa dampo litarahisisha utupaji taka kwa wakazi wa eneo la boko, mabwepande, bunju, kawe na mwenge.
Kauli hiyo ya DC Hapi imekuja baada ya kutembelea na kukagua eneo hilo ambalo awali wachimbaji wake walipewa amri ya kutokuendelea na uchimbaji wa kokoto, lakini baadhi wamekaidi amri hiyo na kuendelea.
Akielezea zaidi Hapi amewataka kutokuendelea kuchimba na hasa katika kipindi hiki cha mvua, kwani wanaweza kujisababishia madhara ya kufukiwa na kifusi na kupoteza uhai.
Amesema amewaelekeza maafisa mazingira na mipango miji wa manispaa waunde timu ,waangalie uwezekano wa kuweka dampo kwenye eneo hilo, kwani eneo la dampo lililopo ni moja Pugu Kinyamwezi, ambako ni mbali.
Aidha amesema dampo hilo lifanywe la kisasa ili uwe mradi ambao utasaidia kuingiza mapato kwa manispaa.
Aidha HAPI ameeleza kuwa pindi eneo hilo litakapoanza kutengenezwa watu waliokuwa wakichimba hapo waandae orodha ya majina ili mawe yatakayotolewa hapo wapewe wao.
Kwa upande wake afisa mazingira wilaya ya kinondoni Mohamed Msangi amesema, eneo hilo likifanywa dampo litarahisisha utupaji taka kwa wakazi wa eneo la boko, mabwepande, bunju, kawe na mwenge.
Eneo
linalochimbwa kokoto na baadhi ya Wakazi wa Boko chama,ambalo kwa sasa
utaratibu wake umesitishwa na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni,Mh.Ally Hapi
Mkuu wa wilaya ya Kinondoni Ally Hapi akiwa na wakazi wa Boko chama katika eneo la uchimbaji wa kokoto
Mkuu wa wilaya ya Kinondoni Ally Hapi
akizungumza na watendaji wa Kata pamoja na wenyeviti wa Serikali za
Mitaa jana katika Ofisi ya Afisa mtendaji wa Kata ya Bunju katika ziara
yake ya siku kumi.
Wenyeviti
wa Serikali za mitaa na watendaji katika Kata ya bunju wakimsikiliza
mkuu wa wilaya ya Kinondoni Ally Hapi jana katika ziara yake.
SHARE
No comments:
Post a Comment