Meneja
Uhusiano wa TTCL, Nicodemus Thom Mushi (kushoto) kwa niaba ya Afisa
Mtendaji Mkuu wa TTCL, akikabidhi msaada wa Vyakula, Vinywaji na
mahitaji mengine ya nyumbani kwa wawakilishi mbalimbali wa vituo vya New
Life Orphanage home cha Boko na Kituo cha Sifa Group Foundation cha
Vikawe Bondeni vyote vya jijini Dar es Salaam.Meneja
Uhusiano wa TTCL, Nicodemus Thom Mushi (wa kwanza kulia) kwa niaba ya
Afisa Mtendaji Mkuu wa TTCL, akikabidhi msaada wa Vyakula, Vinywaji na
mahitaji mengine ya nyumbani kwa wawakilishi mbalimbali wa vituo vya New
Life Orphanage home cha Boko na Kituo cha Sifa Group Foundation cha
Vikawe Bondeni vyote vya jijini Dar es Salaam.Meneja
Uhusiano wa TTCL, Nicodemus Thom Mushi (kushoto) kwa niaba ya Afisa
Mtendaji Mkuu wa TTCL, akikabidhi msaada wa Vyakula, Vinywaji na
mahitaji mengine ya nyumbani kwa wawakilishi mbalimbali wa vituo vya New
Life Orphanage home cha Boko na Kituo cha Sifa Group Foundation cha
Vikawe Bondeni vyote vya jijini Dar es Salaam.KAMPUNI ya Simu Tanzania TTCL imetoa msaada wa
Vyakula, Vinywaji na mahitaji mengine ya nyumbani ili kuwawezesha Watoto
katika Vituo vya Yatima na Waishio katika Mazingira magumu kusherehekea
Siku kuu ya Eid. Akikabidhi msaada huo kwa niaba ya Afisa Mtendaji Mkuu wa TTCL,
Meneja Uhusiano wa TTCL Ndg Nicodemus Thom Mushi amesema, TTCL
inathamini sana makundi yenye mahitaji maalumu kama Yatima ndio maana
mara zote imekuwa mstari wa mbele kuwasaidia kadiri uwezo wa Kampuni
unavyoruhusu. “Nawaomba mpokee salamu za Afisa Mtendaji Mkuu wa TTCL Ndg Waziri
Kindamba, anawasalimu na kuwatakia kila la kheri katika kukamilisha
mwezi Mtukufu wa Ramadhani na sherehe njema za Eid. Watoto wanaopata
malezi katika vituo vyenu wana haki sawa na watoto wenye wazazi na
wanaoishi na familia zao. Kwa ushiriano mwema kati yetu, tutawezesha
Watoto hawa kukua salama na kua Raia wema wa nchi yetu na nguzo muhimu
ya maendeleo ya Taifa letu” amesema ndugu Mushi. Picha
ya pamoja na Meneja Uhusiano wa TTCL, Nicodemus Thom Mushi mara baada
ya makabidhiano ya msaada wa Vyakula, Vinywaji na mahitaji mengine ya
nyumbani kwa wawakilishi wa vituo vya New Life Orphanage home cha Boko
na Kituo cha Sifa Group Foundation cha Vikawe Bondeni vyote vya jijini
Dar es Salaam.Picha
ya pamoja na Meneja Uhusiano wa TTCL, Nicodemus Thom Mushi mara baada
ya makabidhiano ya msaada wa Vyakula, Vinywaji na mahitaji mengine ya
nyumbani kwa wawakilishi wa vituo vya New Life Orphanage home cha Boko
na Kituo cha Sifa Group Foundation cha Vikawe Bondeni vyote vya jijini
Dar es Salaam.Akishukuru kwa Niaba ya Vikundi vilivyopokea msaada, Mkuu wa Kituo
cha New Life Orphanage home cha Boko Dawasa Bi Mwanaisha Magambo
amesema, Kituo chake chenye watoto 132 kitafaidika sana na msaada huu wa
TTCL uliowafikia wakiwa wamekata tamaa kwa kutopata msaada wowote
katika sherehe hizi. Nawaombea kwa Mungu, Kampuni hii idumu, mfanikiwe
katika malengo yenu yote. Msaada huu ni mkubwa, hatukuutarajia na tulikuwa tumekata tamaa kwa
kuwa maombi yetu yote hayakupata majibu kutoka kwa Wafadhili wetu.
Mmetushika mkono kipindi tulichowahitaji hasa, Mungu awabariki sana
TTCL, msichoke kusaidia kundi hili la watoto lenye mahitaji makubwa ya
msaada hasa wa chakula na vifaa vya Elimu. Msaada wa TTCL umetolewa kwa vikundi Viwili vya New Life Orphanage
Home (Watoto 132) na Kituo cha Sifa Group Foundation cha Vikawe Bondeni
chenye watoto 50. Vifaa vilivyotolewa ni pamoja na Mchele kg 300, Unga
wa mahindi kilo 300, Unga wa Ngano kg 200, Sukari kg 200, Maharage kg
200, Mafuta Ndoo 6, Mbuzi 2, Soda katoni 40, Maji Katoni 40, Juice
Katoni 80 na Viungo mbalimbali vya chakula na vifaa vya nyumbani kama
mafuta ya kujipaka na Sabuni.
No comments:
Post a Comment