TRA

TRA

Saturday, September 9, 2017

Uturuki yamkodolea macho Diego Costa

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !
Klabu ya Fenerbahce ya Uturuki imefanya mazungumzo na wawakilishi wa mshambuliaji wa Chelsea Diego Costa kuhusu uwezekano wa kumchukua kwa mkopo.

Costa, 28, amesalia nchini Brazil na amekataa kurejea England.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Uhispania alishindwa kuhama kutoka kwa mabingwa hao wa Ligi ya Premia kabla ya siku ya mwisho ya kuhama wachezaji katika ligi nyingi kuu Ulaya.
Hata hivyo, dirisha la uhamisho wa wachezaji Uturuki bado liko wazi na litafungwa baadaye leo Ijumaa.

 Diego Costa alifungia Chelsea mabao 20 msimu uliopita

Duru zinasema baada ya mazungumzo ya kwanza kufanyika, uwezekano wake kuhama ni finyu, lakini mazungumzo bado yanaendelea.
Costa ameambia na meneja wa Chelsea Antonio Conte ajitafutie klabu itakayomchukua.

Alitaka kurejea Atletico Madrid majira ya joto lakini klabu hiyo ya Uhispania hairuhusiwi kuwasajili wachezaji kutokana na marufuku waliyowekewa hadi Januari.

Hii ina maana kwamba Costa anaweza tu kuhamia klabu hiyo Januari mwakani.
Mshambuliaji huyo hajajumuishwa kwenye orodha ya wachezaji wa Chelsea watakaoshiriki Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya.

CHANZO: BBC

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger