TRA

TRA

Saturday, September 9, 2017

Mbio za magari za milimani zaanza Rwanda

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !



Mashindano ya mbio za magari ya Rwanda Mountain Rally yameanza kutimua vumbi dereva kutoka Kenya Manvir Singh akitarajia kushinda na kuwa bingwa wa Afrika.
Dereva kutoka Kenya Manvir Singh anayeendesha gari aina ya Skoda amefanya vyema katika raundi zilizofanyika asubuhi na kuwatisha wapinzani wake.

Mizunguko ya leo ilikuwa kwenye barabara mbovu za upande wa mashariki mwa Rwanda walipozunguka kilomita 74 mara mbili.
 Mkenya Manvir Singh amefanya vyema asubuhi

Dereva kutoka Zambia Leroy Gomez akiendesha gari aina ya Mitsubishi amejaribu kutoa upinzani mkali licha ya kupata matatizo ya gari yake kupinduka lakini akaweza kuendelea na mashindano.

Dereva mwingine anayefanya vyema ni Bukera Valery, bingwa mtetezi wa mashindano haya kutoka Burundi akiwa katika gari aina ya Subaru Impreza.
Jumla ya magari 16 yameanza mashindano haya yatakayodumu kwa siku tatu.
Dereva huyo kutoka Kenya Manvir Singh akiwa anahitaji alama 25 za shindano hili la Rwanda ili kutangazwa bingwa wa Afrika kabla hata ya shindano la mwisho litakalofanyika Zambia. 

CHANZO: BBC

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger