TRA

TRA

Wednesday, November 8, 2017

Mfuko wa LAPF unahitaji pongezi, wengine waige

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !



MFUKO wa Pensheni wa LAPF umekuwa mstari wa mbele kutoa misaada mbalimbali kwa jamii ili kuharakisha maendeleo ya nchi na watu wake.

Mfano wa hivi karibuni ni namna mfuko ulivyoitikia mwito kuchangia fedha kwa ajili ujenzi wa ofisi za kisasa za walimu katika mkoa wa Dar es Salaam.

Itakumbukwa kuwa ukosefu wa ofisi za walimu nchini ni tatizo kubwa ndiyo maana Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amebuni mbinu ya kujikwamua na bila kuchukua muda mrefu LAPF wakajitokeza haraka kusaidia.

LAPF walitoa fedha taslimu Sh. Milioni 5 kwa mkuu huyo wa mkoa ili kuhakikisha suala la ujenzi wa ofisi za kisasa kwa walimu mkoani humo linafanyika kwa haraka ili waweze kuandaa ratiba/vipindi vya wanafunzi vizuri.

Mchango ulitolewa kwa Mkuu wa Mkoa na Meneja Mawasiliano na Masoko wa LAPF,  James Mlowe kwa ajili ya kununulia mifuko 500 ya saruji katika kuchangia kampeni ya ujenzi wa ofisi hizo za walimu kwa shule za msingi na sekondari.


Meneja Mawasiliano na Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa LAPF, James Mlowe akizungumza wakati wa tukio la kukabidhi msaada wa fedha kwa ajili ujenzi wa ofisi za kisasa kwa walimu wa shule za msingi na sekondari kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda


Ifahamike kuwa kampeni hiyo ilianzishwa na Makonda katika jijini la Dar es Salaam, ambapo  ofisi zaidi ya 400 zitajengwa katika shule za jiji la Dar es salaam hivyo  kuboresha utendaji kazi wa walimu hao.

Kimsingi LAPF imeonesha njia na wadau wengine wanatakiwa kuiga kwa kutoa misaada ya aina hiyo ili kukuza maendeleo ya nchi hususan kwenye sekta ya elimu kwani ndiyo mkombozi kwa watoto wetu. 

Hii ina maana kuwa viongozi wa LAPF wameonesha kuwa wanathamini sekta ya elimu kwa kiwango kikubwa.
 

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger