TRA

TRA

Saturday, May 28, 2016

DUA YA KUWAOMBEA WALIOUWAWA KATIKA MSIKITI WA R RAHMAN IBANDA

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !



1
Mohamed  Taqi Khan  (20) raia wa Jamhuri ya Watu wa Iran akionyesha uwezo na  kipaji chake cha kuhifadhi Quraan tukufu katika uwanja wa shule ya Msingi Mbugani  katika Wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza.Ana uwezo wa kutumia njia 52 kuelezea Quraan.Waliomshikia vinasa sauti (Microphone) kulia ni Sheikh Ramadhan Hashimu na kushoto ni Mohamed Naqi Taqi.
2
Mohamed Naqi Khan (20)  akionyesha kipaji na uwezo wake wa kuelezea Quraan ambayo  ameihifadhi kichwani akiwa na umri wa miaka 10, miaka saba baada ya wazazi wake kufariki dunia na antumia njia 52 kuelezea Quraan hiyo. Hapa akionyesha kipaji chake hicho kwenye uwanja wa Shule ya Msingi Mbugani Jijini Mwanza na kutokana na kipaji chake hicho amekuwa kivutio kwa maelfu ya waumini wa dini ya Kiislamu akiwa ameendesha vipindi zaidi 2000 katika nchi za Kiislamu katika miji mbalimbali.
3
KATIBU wa Bakwata wa Mkoa wa Mwanza Mohamed Salum Balla akizungumza baada ya dua maalumu ya kuwaombea waumini wa dini ya kiislamu waliouawa wakiswali katika msikiti wa R Rahman Ibanda Relini.Dua hiyo ilisomwa katika Uwanja wa shule ya Msingi Mbugani jijini Mwanza juzi na kuhudhuriwa na Sheikh Mkuu wa mkoa wa Mwanza, Alhaji Salum Ferej wa pili kulia kwa Balla wa pili ni Sheikh Hassan Kabeke ambaye ni Mwenyekiti mwenza wa Amani na wa pili kutoka kulia ni Mwenyekiti wa wa Bodi ya wadhamini ya TIC Dk. Mohamed Kanju .
4
Katibu wa Bakwata wa Mkoa wa Mwanza Mohamed Salum Balla akizungumza baada ya dua maalumu ya kuwaombea waumini wa dini ya kiislamu waliouawa wakiswali katika msikiti wa R Rahman Ibanda Relini.Dua hiyo ilisomwa katika Uwanja wa shule ya Msingi Mbugani jijini Mwanza juzi na kuhudhuriwa na Sheikh Mkuu wa mkoa wa Mwanza, Alhaji Salum Ferej wa pili kulia kwa Balla wa pili ni Sheikh Hassan Kabeke ambaye ni Mwenyekiti mwenza wa Amani na wa pili kutoka kulia ni Mwenyekiti wa wa Bodi ya wadhamini ya TIC Dk. Mohamed Kanju ,Alhaji Sibtain Meghjee ambaye ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Bilal Muslim Mission of Tanzania, wa kwanza kulia.
Picha zote na Baltazar Mashaka (P.T)

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger