RAIS
Mstaafu wa awamu ya Pili, Alhaj Dk. Ally Hassan Mwinyi akisoma hotuba
yake wakati alipozindua kongamano la tatu la Taasisi za Kifedha za
Kiislam Afrika, lenye lengo la kujengeana uwezo na wadau wa sekta za
kifedha kwa watendaji wa taasisi hizo linalofanyika kwenye hoteli ya
Hyyat Regency kwa siku mbili.
Baadhi ya
wadau wakiwa katika Kongamano la tatu la Taasisi za Kifedha za Kiislam
Afrika, lenye lengo la kujengeana uwezo na wadau wa sekta za kifedha
kwa watendaji wa taasisi hizo.
Baadhi ya wasiriki wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya uzinduzi huo.
RAIS Mstaafu wa awamu ya Pili, Alhaj Dk. Ally Hassan Mwinyi akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa kongamano hilo.
RAIS
Mstaafu wa awamu ya Pili, Alhaj Dk. Ally Hassan Mwinyi, amesema kuwa
benki zimekuwa zikiendeshwa kwa kutoa mkopo bila riba hivyo itasaidia
watanzania kujiwekea akiba na kuweza kukopa kwa ajili ya maendeleo yao
.
Mwinyi a
ameyasema hayo leo , wakati akifungua kongamano la tatu la Taasisi za
Kifedha za Kiislam Afrika, lenye lengo la kujengeana uwezo na wadau wa
sekta za kifedha kwa watendaji linalofanyika kwenye hoteli ya Hyyat
Regency kwa siku mbili katika kuwezesha urahisishaji wa usimamizi wa
taasisi hizo na fursa ambazo wanaweza kuwekeza katika nchi za Afrika
ikiwemo na Tanzania.
Amesema
zipo baadhi ya benki zinatoza riba kubwa, hali inayowafanya wananchi
baadhi ya wananchi kujiunga taasisi za kifedha na kuogopa kukopa
mikopo kitokana na riba wanazotoza.
Aidha amewawahamasisha wananchi kujiunga na benki za kiislaam ili kujiwekea akiba na kukopa fedha bila riba.
Nae
Mkurugenzi wa Masoko kutoka Bima ya Kiislam Zanzibar, Said Abdallah,
amesema asilimia 15 ya wananchi wanaojiunga na mfumo mpya wa bima ya
Kiislam ni wapya.
“Kuna
umuhimu ya kuanzisha bima nyingine za kiislam nchini katika kuwezesha
wananchi kujiunga na bima kwa ajili ya maisha yao,”amesema Rais
Mstaafu, Mwinyi.
Amesema
pia sheria ya kuandaa bima za kiislam ni changamoto kubwa na kwamba
hawajapata kibali kwa kamishina wa Bima tangu wameanza kufuatilia mwaka
2008 .(P.T)
SHARE








No comments:
Post a Comment