Waziri wa
Afya Zanzibar Mahmoud Thabit Kombo akizungumza na wafanyakazi katika
hafla ya kuamuaga Katibu Mkuu aliemaliza muda wake Dkt. Mohd Jidawi
(kushoto) na kumkaribisha Katibu Mkuu mpya (kulia) Dkt. Juma Malik Akili
alievaa kofia katika Ofisi ya Wizara hiyo Mnazimmoja, Mjini Zanzibar.
Katibu
Mkuu Mstaafu wa Wizara ya Afya Dkt. Mohd Jidawi akiwashukuru wafanyakazi
wa Wizara hiyo kwa ushirikiano mkubwa waliompa wakati wa kutekeleza
majukumu yake.
Waziri wa
Afya Mahmoud Thabit Kombo na Katibu Mkuu mpya wa Wizara hiyo Dkt. Juma
Malik Akili wakimsikiliza katibu Mkuu mstaafu Dkt. Mohd Jidawi (hayupo
pichani) wakati wa hafla ya kumuaga iliyofanyika Wizara ya Afya
Mnazimmoja.
Waziri wa
Afya Mahmoud Thabit Kombo akimkabidhi cheti cha heshima Katibu Mkuu
mstaafu wa Wizara hiyo Dkt. Mohd Jidawi katika hafla ya kumuaga
iliyofanyika Wizarani, Mnazimmoja. Wa kwanza (kushoto) ni mke wa Dkt.
Jidawi, Dkt. Mwanaheri Jidawi.
Waziri wa
Afya Mahmoud Thabit Kombo akimkabidhi meza yenye mlango wa Zanzibar
(Zanzibar Door), Katibu Mkuu mstaafu wa Wizara hiyo Dkt. Mohd Jidawi
katika hafla ya kumuaga iliyofanyika Wizarani, Mnazimmoja. Wa kwanza
(kushoto) ni mke wa Dkt. Jidawi, Dkt. Mwanaheri Jidawi.
Waziri wa
Afya Mhmoud Thabit Kombo, Katibu Mkuu mstaafu na Katibu Mkuu mpya
katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi walioshiriki katika
hafla hiyo. Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar.(P.T)
SHARE








No comments:
Post a Comment