TRA

TRA

Saturday, October 29, 2016

TCRA WAWAJENGEA UWEZO ASKARI POLISI WA KITETO JUU YA KUPAMBANA NA UHALIFU WA MITANDAONI

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


h4
Mkuu wa kituo cha polisi Kibaya Patrick Kimaro (sabasita) akizungumza kwenye mafunzo hayo.
h3
h2
Wafanyakazi wa TCRA Kanda ya Kaskazini wakiendesha mafunzo hayo
h1
Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Mkoani Manyara, Tumaini Magessa (kulia) na mkuu wa polisi wa wilaya hiyo Fadhili Luoga wakifutilia mafunzo hayo.
Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Mkoani Manyara, Tumaini Magessa amewaasa askari polisi kuwachukulia hatua kali wahalifu wa mitandao ili kukomesha matukio hayo ambayo yamekuwa kero kwa jamii katika sehemu tofauti hapa nchini.
Magessa alitoa kauli hiyo wakati akifungua mafunzo ya maofisa wa polisi wilaya ya Kiteto juu ya masuala ya uhalifu wa mitandao, yaliyoandaliwa na mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA) kanda ya kaskazini na kufanyika kwenye jumba la maendeleo ya jamii mji mdogo wa Kibaya.
Alisema ukuaji wa teknolojia umewezesha kupata mawasiliano ya intaneti kupitia simu, kutuma na kupokea fedha kwa kutumia simu za mikononi na kulipia huduma mbalimbali ila baadhi ya watu wanatumia matumizi hayo vibaya hivyo wachukuliwe hatua kali.
Alisema maendeleo ya matumizi ya simu yamekuja na changamoto hizo pamoja na matumizi mabaya ya teknolojia ya mawasiliano na baadhi ya watumiaji wameibiwa pesa kwenye akaunti zao za fedha kupitia mitandao.
Meneja wa TCRA kanda ya kaskazini Annette Matindi alisema kuna aina nyingi za uhalifu kupitia mitandao ya simu na intaneti ikiwemo kutokusajili laini za simu au kutumia majina bandia kusajili simu.
Matindi alitaja makosa mengine ni kutumia simu kutuma ujumbe wa matusi au kasha na vitisho, utapeli na wizi wa fedha kupitia mtandao na simu ikipoteza mawasilino kwa muda pindi yakirudi unakuta fedha zimeibiwa.
Mkuu wa Kituo cha polisi Kibaya, ASP Patrick Kimaro (Sabasita) alitoa wito kwa jamii kuzingatia na kusisitiziwa kuwa na matendo ya uadilifu ili kukomesha matukio ya makosa ya mitandaoni kupitia ulimwengu huu wa teknolojia.
Kimaro alisema watumiaji wa mitandao ya kijamii wanapaswa kutambua kuwa wakitumiwa picha, sauti au maneo ya kashfa, uchochezi au udhalilishaji, wanapaswa kutoa taarifa kwenye kituo cha polisi ili kukomesha hali hiyo.
Alisema kusambaza picha, sauti au maneno yenye viashiria vya makosa ya mtandao kwa kisingizio kuwa umetuliwa na mtu hakusababishi mtu asichukuliwe hatua hivyo wanapaswa kufuta kuliko kusambaza.
Pia, alisema mafunzo kama hayo yanapaswa kutolewa mara kwa mara kwa askari polisi ili waendelee kukomesha makosa hayo kwani vijana wengi wenye utaalamu wa kompyuta na suala la IT wanajifunza mbinu mpya kila mara za ualifu wa mitandao.
Kwa upande wake, askari wa kituo hicho Bkari Yusuf alisema kwa sababu TCRA wana uwezo wa kuzima simu feki, pia watu wanaotumia mitandao ya kijamii kwa kuvunja maadili wanapaswa kufungiwa ili kukomesha makosa hayo.(P.T)

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger