TRA

TRA

Saturday, October 29, 2016

AZAM FC YAILAZA KAGERA SUGAR 3-2 MCHEZO WA VPL,BOCCO AOKOA JAHAZI LA WAHISPANIA

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


fb_img_1462443984306
Na.Alex Mathias.
Kikosi cha Azam FC kimepeleka maumivu tena kwa timu ya Kagera Sugara baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-2 mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara uliochezwa kwenye uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba.
Wenyeji walikuwa wa kwanza kupata bao kupitia kwa mshambuliaji wao hatari Themi Felix dakika ya 32 kutokana uzembe wa mabeki wa wageni hata hivyo halikudumu kwani kiungo mshambuliaji Mudathir Yahya kusawazisha dakika ya 40 hadi mapumziko timu hizo zilikwenda nguvu sawa.
Kipindi cha pili kilianza kwa kushambuliana alikuwa Themi Felix alifunga la pili dakika ya 68 kwa njia ya mkwaju wa penati baada ya Agrey Moris kuunawa mpira ndani ya 18 baada ya kuingia kwa bao hilo kuliamsha hasira kwa Azam Fc na kulisakama lango la wenyeji.
Mchezaji wa zamani wa Yanga,Frank Domayo aliisawazishia timu yake kunako dakika ya 80 kwa shuti kali lililomshinda mlinda mlango na Nahodha wa Azam alipeleka Maumivu kwa Kagera Sugar, John Bocco kwa kufunga la tatu na la ushindi dakika ya 86 hadi mpira una malizika Azam FC wameibuka na ushindi wa magoli 3-2.
Kwa matokeo hayo Azam FC wamepanda hadi nafasi ya nne wakiwa na alama 19 katika msimamo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara wakati Kagera Sugar wameendelea kuugusa maaumivu kwa kufungwa mechi ya pili kwani Mchezo uliopita walikubali kuchakazwa kwa aibu na Yanga cha magoli 6-2 na kushuka hadi nafasi ya tano wakibaki na alama 18. (P.T)

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger