Muhubiri TB Joshua amesema kuwa Bi Clinton atashinda kwa ushindi mdogo dhidi ya mpinzani wake
Muhubiri
maarufu wa vipindi vya Televisheni nchini Nigeria TB Joshua amesema
ametabiri " kwamba Hillary Clinton atamshinda Donald Trump" katika
uchaguzi wa urais wenye ushindani mkali tarehe 8 Novemba mwaka huu.
Katika
ujumbe alioutuma kwenye ukurasa wake wa Facebook TB Joshua amesema kuwa
Bi Clinton atashinda kwa ushindi mdogo, lakini atakabiliwa na changamoto
nyingini - likiwemo jaribio la kupiga kwa kura ya kutokuwa na imani
dhidi yake.
"boti ya rais mpya itakuwa imefungwa," aliongeza.
TB Joshua
ni mmoja wa viongozi wa kidini wenye ushawishi na utata barani Afrika,
huku wengi wa wafuasi wake wakiamini kuwa "utabiri " wake ni wa uhakika.BBC
SHARE








No comments:
Post a Comment