Donald Trump na Hillary Clinton wagombea katika uchaguzi wa urais Marekani, Novemba 8, 2016.
Wananchi
wa Marekani watapiga kura leo Jumanne kumchagua rais wao, ambaye
atamrithi Rais Barack Obama. Wagombea katika uchaguzi huo ni Donald
Trump wa chama cha Republicana na Hillary Clinton wa chama cha
Democratic.
Uchaguzi
huu umekua na ushindani mkubwa tangu kuanza kwa kampeni za uchaguzi
mpaka siku ya leo ya uchaguzi watu wameendelea kutoa tathmini zao kuhusu
nani ataibuka mshindi.
Awali
wagombea hawa wawili walionekana katika mijadala kwenye runinga
wakitupia vijembe na kila mmoja kumshutumu mwengine kwa makosa
aliyofanya kwamba hana hadhi ya kuliongoza taifa la Marekani.
Hata
hivyo uamuzi wa mwisho wa mshindi wa urais nchini Marekani huamuliwa na
wajumbe 538 wanaoteuliwa kutoka katika majimbo yote 50 nchini humo.
Hatua hii
huja mara baada ya raia wa kawaida kupiga kura katika vituo mbalimbali
na kumchagua rais wao wanaotaka awaongoze kwa muda wa miaka minne.
Mgombea
anastahili kupata angalau kura 270 za wajumbe kati ya 538 ili kuwa rais
wa Marekani na wajumbe hao huamua mshindi kwa namna watu walivyopiga
kura katika majimbo mbalimbali.
Wakati wa
uchaguzi wa mwaka 2012, Barrack Obama alipata ushindi baada ya
kuchaguliwa kwa kupata kura 65,915,795 huku mpinzani wake Mitt Romney
akipata kura 60,933,504.
Wajumbe walipopiga kura, Obama alipata ushindi wa wajumbe 332 dhidi ya Romney aliyepata kura ya wajumbe 206 katika uchaguzi huo.
Kuelekea Uchaguzi huu, kuna majimbo ambayo ni ngom
SHARE








No comments:
Post a Comment