TRA

TRA

Thursday, August 24, 2017

NJOONI RUKWA CHAKULA "BWERERE"; RC ZELOTE STEVEN

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !



NA MWANDISHI WETU, RUKWA
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Kamishna wa Polisi (mstaafu) Zelote Stephen ameialika mikoa yote nchini yenye upungufu wa chakula kwenda mkoani kwake, kwani kipo cha kutosha.
Ameyasema hayo wakati akifungua mafunzo ya kilimo cha kisasa yaliyoshirikisha uongozi wa Mkoa, Wilaya na Halmashauri zake katika shamba la Msipazi lenye ukubwa wa ekari 4,420 lililopo katika Kijiji cha China, Kata ya Kate,Wilayani Nkasi linalomilikiwa na Bw.Salum Summry.
Mkoa wa Rukwa umevuna tani milioni 1.1 za chakula, huku zao la mahindi pekee likiwa limeongoza kwa kuvunwa jumla ya tani 710,652.
Pia amewaomba wakuu wa mikoa kuwahamasisha wafanyabiashara kwenye mikoa yao wafike Mkoani Rukwa kununua bidhaa hiyo ili kuwaondolea hofu wakulima wa mkoani kwake, ya kukosa wateja na hivyo kuanza mikakati ya kuuza chakula nje ya nchi.
 “Nichukue nafasi hii kuthubutu kuiambia mikoa mingine ambayo haijapata bahati ya kuvuna kama tulivyovuna sisi watumie fursa hii watuambie kupitia ngazi zilizopo kwamba wanahitaji nini, hili ni kwa Tanzania bara na visiwani, tunawakaribisha kufanya biashara na sisi,” Alisema Mkuu wa Mkoa.
Hata hivyo amewaasa wananchi wa mkoa huo, kutouza chakula chote na kwamba waweke akiba kwani serikali haitatoa chakula cha msada kutokana na njaa.
“Sisi siyo wachoyo, uchoyo wetu ni kuhakikisha wananchi wetu wanakuwa na akiba ndani ya nyumba zao, na wale wanaouza mazao wahakikishe wanatenga fedha zinazotokana na mauzo hayo kwaajili ya kununua pembejeo za msimu wa kilimo unaofuata,” Amesema
Katika kuhakikisha wakulima wanaondokana na adha ya mbegu feki na ubabaishwaji wa bei za pembejeo Mh. Zelote amewaagiza wauzaji wa pembejeo hizo kuweka mabango ya bei nje ya maduka yao na kuwaagiza wakuu wa wilaya kuwachukulia hatua wale wote watakaogundulika kuuza mbegu feki.
Mbali na hayo Mh. Zelote amesema kuwa anataka kusikia mkoa wa Rukwa unakuwa wa kwanza nchini kwa uzalishaji wa chakula baada ya kuwa wa tatu ukitanguliwa na Ruvuma na Mbeya, hivyo aliwataka wale ambao hawalimi kuonja utamu wa kilimo kwa kulima japo ekari moja.
“Naambia Mkoa wa Mbeya umekuwa wa Kwanza, tujiulize wametuzidi nini, mkoa wa Ruvuma umekuwa wa Pili, wametuzidi nini, sasa mwaka huu nataka kusikia mkoa wa Rukwa umekuwa wa kwanza ama wote watatu tushike namba moja,” alimalizia.
Awali alipokuwa akisoma taarifa ya shammba hilo, Mkurugenzi wa Shamba la Msipazi Salum Summry amesema kuwa miongoni mwa changamoto zinazorudisha nyuma juhudi za wakulima katika Mkoa wa Rukwa ni uwepo wa mbegu zisizo na ubora “Fake” pamoja na wadudu waharibifu wa mazao.
“Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa suala la mbegu feki limekuwa likirudisha nyuma juhudi zetu kama wakulima ambao tunaanza kuchipukia, na pia msimu huu tulishambuliwa na wadudu jamii ya viwavi jeshi lakini nichukue nafasi hii kukushukuru wewe binafsi, Mkuu wa Wilaya ya Nkasi pamoja na Mkurugenzi wa Halmashauri kwa mlivyotusaidia kukabiliana na wadudu hao kwa kuwezesha kupata ndege ya kunyunyizia madawa n ahata mafuta ya ndege kwaajili ya kazi hiyo,” Salum Summry alisema.
Naye Mstahiki Meya wa manispaa ya Sumbawanga Mh. Justin Malisawa alimshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kuwahamasisha wananchi wa Rukwa kulima na kuongeza thamani katika mazao yao.



 Mfanyabiashara na mwekezaji katika kilimo, Bw. Salum Sumry, (kushoto), akifafanua jambo mbele ya Mkuu wa Mkoa, Mhe. Zelothe Steven, (mwenye miwani), na Katibu Tawala wa Mkoa huo, Bw.Makali, wakati Mkuu wa Mkoa na ujumbe wake, walipotembelea shamba la Msipazi lenye ukubwa wa ekari 4,420 lililopo katika Kijiji cha China, Kata ya Kate,Wilayani Nkasi

Mkuu wa Mkoa akifafanua jambo baada ya kutembelea shamba la Bw. Sumry.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger