Chama Cha Mapinduzi kimeitaka
Serikali kuchukua hatua za haraka kuhusu matukio ya Mauaji yanayoendelea
katika Wilaya za Kibiti, Mkutanga na Rufiji Mkoani Pwani ili kuepusha
mauaji hayo kuendelea kutokea.
Katibu wa NEC, Itikadi
na Uenezi, HUMPHEY POLEPOLE, amesema hayo Jijini Dar es salaam jana
wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mauaji yanayoendelea
katika Wilaya hizo.
POLEPOLE pia amevitaka
vyombo vya ulinzi na usalama kuhakikisha vinaelekeza akili, nguvu zao
katika Wilaya hizo kwa kuwa maujia hayo yanasababisha kuzorota kwa
shughuli za maendeleo.
Amesema chama kwa muda
mrefu kimekaa kimya kikiamini hatua zitachukuliwa kwa kuwa wanachama
wake na watendaji wameendelea kupoteza maisha ambapo amesema kwa sasa
imetosha.
Kuhusu suala la uchaguzi ambao
unaendelea ndani ya Chama hicho amesema mauaji hayo yanakiweka Chama
katika mazingira magumu ya kufanya chaguzi zake hivyo ni vema hatua
zikachukuliwa sasa.
Katika hatua nyingine,
POLEPOLE amesema Chama kimeipongeza Kamati Maalum ya kuchunguza Mchanga
wa Madini kwa kazi nzuri iliyofanywa sanjari na kuwaomba wananchi
kumuunga mkono Rais JOHN MAGUFULI kwa hatua alizozichukua kwa watendaji
kutokana na Ripoti ya Mchanga wa Madini.
SHARE








No comments:
Post a Comment