TRA

TRA

Friday, August 4, 2017

Manji ashindwa kufika mahakamani

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !
August 4, 2017 Mfanyabiashara Yusuf Manji anayekabiliwa na tuhuma za kesi ya uhujumu uchumi ameshindwa kufika katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa sababu ana kesi nyingine Mahakama Kuu.
Hayo yameelezwa mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi baada ya Wakili wa Serikali, Mutalemwa Kishenyi, kueleza kesi imeitishwa kwa ajili ya kutajwa, na upelelezi wa kesi haujakamilika lakini Mshtakiwa wa kwanza ambaye ni Manji ameshindwa kwa sababu ana kesi nyingine Mahakama Kuu.
Baada ya kuelezwa hayo, Hakimu Mashauri aliahirisha kesi hiyo hadi Agosti 9, 2017 kwa ajili ya kutajwa ingawa washtakiwa wenzake ambao ni Deogratias Kisinda, Abdallah Sangey na Thobias Fwele wamefika mahakamani.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger