MAHAKAMA
ya Hakimu Mkazi Kisutu leo Agosti 25, 2017 imemtia hatiani
mfanyabiashara Yusuf Manji katika kesi ya kutumia dawa za kulevya aina
ya heroin. Ataanza kujitetea Agosti 30 na 31, mwaka huu.
Uamuzi huo umetolewa na Hakimu Mkazi Mfawidhi Cyprian Mkeha, wakati kesi hiyo ilipoitishwa kwa ajili ya kutolewa uamuzi.
Hakimu
Mkeha alisema kuwa ameridhika na ushahidi uliotolewa na mashahidi wa
upande wa mashtaka na kwamba mshtakiwa ana haki ya kujitetea kutokana na
mkojo wake kukutwa na dawa aina ya morphine ambayo zao lake ni heroin.
“Hivyo mshtakiwa anapaswa kujitetea kwa sababu Mahakama imemkuta na hatia,”
Baada
ya kueleza hayo, Wakili wa utetezi Hudson Ndusyepo alidai kuwa
mshtakiwa atajitete kwa hati ya kiapo ambapo watakuwa na mashaidi 15.
Hakimu Mkeha aliahirisha kesi hiyo hadi Agosti 30 na 31, 2017 na itasikikizwa mfululizo.
SHARE








No comments:
Post a Comment