TRA

TRA

Friday, August 19, 2016

Riek Machar akimbilia jijini Kinshasa, DRC

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


media
Riek Machar alipowasili mwezi Aprili tarehe 26 mwaka huu .
Makamu wa rais wa zamani wa Sudan Kusini ambaye pia alikuwa kiongozi wa waasi Riek Machar, amekimbilia nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Mshirika wa karibu wa Machar amethibitisha kuwa kiongozi wao amewasili jijini Kinshasa na anataka kwenda nchini Ethiopia haraka iwezekanavyo.
Machar alikimbilia mafichoni kutoka mji mkuu Juba baada ya kuzuka kwa mapigano kati ya wanajeshi wake na wale wa rais Salva Kiir mwezi uliopita karibu na Ikulu ya rais.
Baada ya Machar kuondoka jijini Juba na kukimbilia katika eneo lisilofahamika, rais Kiir alimteua Taban Deng Gai aliyeongoza ujumbe wa upinzani kufanikisha mazungumzo ya amani kati ya waasi na serikali kuchukua nafasi yake, uteuzi ambao Machar alipinga na kusisitiza kuwa anaendelea kuwa Makamu wa kwanza wa rais.
Gai amekuwa ziarani nchini Kenya wiki hii na akizungumza na wanahabari siku ya Jumanne jijini Nairobi, alimtaka Machar kuachana na siasa ili serikali itekeleze ipasavyo mkataba wa amani.
Wiki iliyopita Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lilipitisha azimio la kutuma kikosi cha wanajeshi 4000 cha kulinda amani kutoka mataifa ya Kenya, Rwanda na Ethiopia kwenda kulinda amani jijini Juba na kuhakikisha kuwa maeneo ya Umoja wa Mataifa hayavamiwi.
Kiir na Machar wameendelea kulaumiana kuhusu mzozo mpya uliotokea katika nchi yao baada ya kuanza kufanya kazi pamoja mwezi Aprili mwaka huu.
Mapigano nchini Sudan Kusini yaliyoanza rasmi mwezi Desemba mwaka 2013 jijini Juba, yamesababisha vifo vya maelfu ya watu na wengine zaidi ya Milioni 2.5 kukimbia makwao. RFI

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger