TRA

TRA

Sunday, August 21, 2016

Santos achaguliwa tena kuongoza chama tawala Angola

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


santo
Jose Eduardo dos Santos amekuwa madarakani kwa miaka 36
Rais wa Angola, Jose Eduardo dos Santos aliyeongoza kwa miaka 36 amechaguliwa tena kuwa kiongozi wa chama tawala cha MPLA.
Uchaguzi wa bunge unatarajiwa kufanywa mwaka ujao, na kiongozi wa chama kinachoshinda ndiye anayekuwa rais.
Rais dos Santos alisema awali mwaka huu, kwamba ataondoka madarakani mwaka wa 2018, lakini ameshawahi kutoa ahadi kama hizo kabla.
Kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 73, analaumiwa kuwa amekusanya madaraka mengi na mali, kwenye mikono ya familia yake na washirika wake wakubwa kisiasa. BBC

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger