TRA

TRA

Monday, March 27, 2017

ARSENAL WATUPWA NJE KOMBE LA FA

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


arsenal-ladies-danielle-carter-jordan-nobbs-alex-scott-fa-cup-win-2015-e1463301393814
Mabingwa watetezi wa Kombe la FA la Wanawake nchini Uingereza, Kina dada wa Arsenal, wametupwa nje ya michuano ya mwaka huu.
Hii ni baada ya kuchapwa 1-0 na kina dada wa Birmingham City katika hatua ya robofainali.
Bao la Birmingham lilifungwa na Marisa Ewers dakika ya 77.
Kipa wa Birmingham Ann-Katrin Berger alifanya kazi ya ziada kuwazuia Arsenal kufunga. Aliokoa makombora kutoka kwa Kim Little, Danielle Carter na Danielle van de Donk kipindi cha kwanza.
Katie McCabe na Jordan Nobbs walishambulia lakini wakashindwa kulenga vyema wavu upande wa Arsenal muda mfupi kabla ya Ewers kufunga. 

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger